Na Sultani Kipingo
Bingwa wa dunia wa masumbi Floyd Mayweather (kushoto) amevuliwa mkanda wa WBO alioupata baada ya kumshinda Manny (kulia)

Pacquiao mwezi Mei Mwaka huu.
Uamuzi huo umekuja baada ya bondia huyo mwenye umri wa miaka 38 kushindwa kuilipa shirikisho la ndondi la WBO ada ya dola laki mbili kabla ya Julai 3, mwaka huu.
Hata hivyo Mayweather mwenyewe alitegemewa kuutema mkanda huo, kufuatia ushindi wa pointi dhidi ya Pacquiao. Mmarekami mwenzie Timothy Bradley ndiye ataepewa mkanda huo.
Baada ya kumshinda Pacquiao, Mayweather alitangaza kwamba angeutema mkanda huo ili kuwapa fursa mabondia wengine vijana kushinda mikanda. 

“Kamati ya mashindano ya dunia ya WBO hina jinsi ila kukoma kumtambua Bw. Floyd Mayweather Jr. kama bingwa wa dunia wa uzito wa welterweight na tunamvua ubingwa huo”, taarifa imesema katika mtandao wa wboboxing.com

Mayweather anategemea kuingia ulingoni tena huko Las Vegas Septemba 12, mwaka huu ingawa bado hajataja atapambana na nani.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...