

Sheikh wa Mkoa wa Dar
es Salaam, Sheikh Alhad Mussa Salum akizungumza mara baada ya kufutari katika futari iliyoandaliwa na Benki ya Finca Microfinance jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. 

Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Benki ya Finca Microfinance, Edward
Greenwood akizungumza na Sheikh wa Mkoawa Dar
es Salaam, Sheikh Alhad Mussa Salum wakati wakifuturu mwishoni mwa wiki.
Baadhi wa waumini wa dini ya Kiislam wakifuturu katika mwenzi Mtukufu wa Ramadhani futari iliyoandaliwa na Benki ya Finca Microfinance jijini Dar es Salam mwishoni mwa wiki
BENKI ya Benki ya Finca Microfinance kwakutambua mchango kwa jamii wanayoihudumia katika mwezi mtukufu wa Ramadhani wammeamua kufuturu na wakazi na wateja wa benki hiyo.
Akizungumza baada yakufuru Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Benki ya Finca Microfinance, Edward
Greenwood amesema wanatambua umuhimu katika mwezi huu kuwa wanawajibu kufuru na watu iliwaendelee kupata baraka yakuendelea kukua kwa benki hiyo.
Amesema kama benki itaendelea kutoahuduma kwani imekuwa ikikua kwa kasi tangu kuanza kama taasisi yamikopo na kuweza kufikia benki ni kutokana na jamii kutambua mchango
wake ambapo imetimiza miaka 18 tangu ilipoanzishwa mwaka 1998.
“Mafanikio haya ya Benki ya Finca Microfinance ni kutokana na mchangowenu
,maoni na ushirikiano wenu bilahivyo tusingewezakufika hapa tulipo”amesema Greenwood.
Nae Sheikh wa Mkoawa Dar
es Salaam, Sheikh Alhad Mussa Salum amesema benki imetambua umuhimu katika mwezi mtukufu kwakutoa sehemu yakufuturisha kwakile wanachokipata.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...