Homa ya michuano ya Kagame inazidi kupamba moto kufuatia vilabu mbalimbali zinazoshirki michuano hiyo kuanza kuwasili jijini Dar es salaam zikiwa na vikosi vyao kamili kwa lengo la kusaka Ubingwa wa michuano hiyo.
APR ya Rwanda tayari imeshawasili jijjini Dar es salaam, pamoja na timu za Al Shandy ya Sudan, KMKM ya Visiwani Znzibar, huku timu za Al Malakia ya Sudan Kusini na mabingwa mara tano wa michuano hiyo Gor Mahia wakitarajiwa kuwasili leo saa saa 10 jioni kwa ndege ya Kenya (KQ).
Kueleka mchezo wa ufunguzi kati ya Yanga dhidi ya Gor Mahia, wenyeji timu ya Yanga (watoto wa Jangwani) wameendelea kujifua katika uwanja wa Polisi Ufundi chini ya kocha wake mholanzi Hans Van der Pluijm na msaidizi wake Mkwasa kuhakikisha wanafanya vizuri katika mechi hiyo.
Gor Mahia ambayo inafundishwa na kocha Frank Nutal raia Skotilandi, inawasili ikiwa na kikosi chake cha kwanza kamili kilichocheza michezo 17 ya Ligi Kuu nchini Kenya bila kufungwa, ikishinda michezo minne na sare michezo mitatu.
Wasifu wa Azam:
Klabu ya Azam ilishiriki kwa mara ya kwanza kwenye michuano ya kombe la Kagame mwaka 2012 lakini walishangaza wengi kwa kumaliza kama washindi wa pili baada ya kufungwa na Yanga mabao 2-0 kwenye mchezo wa fainali.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...