Kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Kingunge Ngombale,Mwilu akizungumza katika mkutano  na waandishi wa habari Dar es Salaam leo ,Kuhusu mkutano mkuu wa  chama hicho uliofayika Dodoma hivi karibuni na mchakato wa kumpata mgombea Urais na  changamoto zilizojitokeza.
Mwanasiasa Mkongwe nchini,Kingunge Ngombale Mwilu akisisitiza jambo mbele ya Waandishi wa habari kutoka vyombo mbalimbali (hawapo pichani) mapema leo,nyumbani kwake makumbusho,jijini Dar.PICHA NA MICHUZI JR.
.
 Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii .

Mwanasiasa   mkongwe nchini,Kingunge Ngombale Mwilu amesema kuwa wanachma wa Chama cha Mapinduzi (CCM) ,umefika wakati muafaka sasa wa kuungana pamoja na kuzika tofauti zao zilikuwa zikijitokeza hapo awali badala yake wasimame imara kukijenga chama chao.

Akizungumza na waandishi habari leo jijini Dar es Salaam,Kingunge amesema CCM inatambulika kimataifa kutokana na historia yake,hivyo lazima kiwe imara wakiwemo viongozi wake wakiwashirikisha na wanachama wao .

Amesema katika uchaguzi wa kutafuta mgombea urais uliofanyika hivi karibuni mkoani Dodoma ulikiuka haki za wagombea kutokana na wagombea kushindwa kwenda katika Mkutano mkuu wa wanachama  na kujieleza.

Kingunge amesema ,kilichotokea Dodoma sio halali na sio haki lakini chama cha CCM lazima kiendelee,alisem na kuongeza kuwa "tumepata mgombea John Magufuli yeye sio aliyefinyanga na wajumbe wa mkutano mkuu,hivyo tumuunge mkono kwa pamoja na kupata ushindi wa kishindo",alisema Kingunge.

"Wana CCM watafute umoja wa kushikamana na kuwa Lowassa ana nafasi ndani ya CCM,hivyo  tuunde mazingira ya kutumia nguvu zilizopo CCM katika kushinda kwa ushindi wa  kishindo katika uchaguzi mkuu",amesema Kingunge.

Amesema yaliyotokea Dodoma lazima yazungumzwe ili watu waweze kutoa duku duku zao kwa kile ambacho kimeonekana katika chama na ni changamoto kubwa ambayo inapaswa kufanyiwa kazi. 
Mwanasiasa Mkongwe nchini na Kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Kingunge Ngombale Mwilu (kushoto) akizungumza katika mkutano  na waandishi wa habari Dar es Salaam leo ,Kuhusu mkutano mkuu wa  chama hicho uliofayika mjini Dodoma hivi karibuni na mchakato wa kumpata mgombea Urais na  changamoto zilizojitokeza

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 16, 2015

    Aibu ng'eeeeeeeeeeeeee

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 16, 2015

    Hata kama uchaguzi ulikiuka haki za wagombea kama anavyodai mzee Kingunge Ngombale Mwilu, kwani lengo lilikuwa ni nini? Si ni kumchagua mgombea ailiyekuwa imara zaidi kuliko wote? Kwani katika wote wale kuna mgombea ailiyekuwa imara zaidi kuliko Dkt. John Pombe Magufuli? Si ni ukweli usiopingika kwamba bila ya kufanyika vile angeweza kiurahisi kuchaguliwa mgombea mwingine ambae angekuwa ni mteremko kwa vyama vya upinzani wakati wa kupiga kura ya uchaguzi wa urais na hatimae kuwepo uwezekano mkubwa wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kushindwa? Waliyotumia njia ile ya kumchagua Dkt. John Pombe Magufuli ambae ndiye imara zaidi kuliko wagombea wengine wote waliona mbali kwa sababu siyo tu yawezekana sana Chama cha Mapinduzi (CCM) kikaendelea kuiongoza nchi yetu endapo Dkt. John Pombe Magufuli atashinda urais bali pia nchi yetu itakuwa imepata kiongozi mchapakazi, asiyekuwa na kashfa na atakaepiga vita ufisadi. Kwa ukongwe wa mzee Kingunge Ngombale Mwilu katika Chama cha Mapinduzi (CCM) na uongozi wa nchi yetu, sikutegemea kabisa kama angeweza kukosoa hadharani mchakato wa namna alivyochaguliwa Dkt. John Pombe Magufuli kwani kwa kufanya kwake hivyo anatoa siri za Chama cha Mapinduzi (CCM) kitu ambacho hakikubaliki na anakwenda kinyume na kauli mbio ya chama chake isemayo "Umoja ni Ushindi". Narudia kusema hata kama uchaguzi ulikiuka haki za wagombea, lakini kwa kuwa aliyechaguliwa ni Dkt. John Pombe Magufuli hicho kwa kweli ni KITENDO KITAKATIFU kutokana na uimara mkubwa wa huyo aliyechaguliwa na maslahi mapana ya Taifa letu na wananchi wetu wote kwa ujumla. Wengi wetu tumefurahi kwa kuchaguliwa Dkt. John Pombe Magufuli kupeperusha bendera ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na tutafurahi zaidi atakaposhinda urais na kuliongoza Taifa letu kama anavyotufurahisha katika kila Wizara anayopewa kuiongoza. Mungu ambariki Rais wetu Mtarajiwa Dkt. John Pombe Magufuli.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 16, 2015

    Huyo mzee hana jipya mimi binafsi sikutegemea mzee kama huyo kwenda kusimama majukwaani hii leo badala ya kuwa mshauri tu.anatia aibu.

    anaacha kupumzika kwa amani leo anasimama majukwaani.walicho dhamilia kimeshindikana.

    Asitake kutuaminisha watz kwamba mtu wao alikua anakubarika kihivyo.Tena bila hata soni eti watanzania wanamhitaji wepi!? mimi binafsi sijawahi kumuhitaji so wasituongelee.

    MZEE KAPUMZIKE HATA NYERERE AKIFUFUKA LEO AKUKUTE JUKWAANI ATAKUSHANGAA SAAAANA!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 16, 2015

    Traitor to the country and the party. GO AWAY Kinguge. Big disappointment.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...