Na Fredy Mgunda,Iringa

Michango hiyo inaendelea katika maeneo ya stendi kuu ya mabasi, stendi ya daladala ya miyomboni, Kihesa, Mtwivila, Kitwiru, Ipogoro na chuo kikuu cha Iringa.
Tangu Kibiki atangaze nia ya kuwania jimbo la Irnga mjini, hali ya upepo wa jimbo hilo imebadilika huku wananchi wakiitaka CCM itende haki badala ya kuwakumbatia wanaotumia rushwa, kutaka madaraka.
Mpaka sasa wanachama wa CCM wanaotajwa kuomba ridhaa ya CCM kuwania jimbo hilo wanafikia 10, akiwemo Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Iringa, Jesca Msmbatavangu na Mjumbe wa halmashauri kuu ya CCM ya jimbo hilo, Mahamud Madenge.
Akizungumza na waandishi wa Habari, Kibiki aliwashukuru wananchi wanaomchangia fedha hizo ili achukue fomu na kuahidi kuwa atafuata kanuni na taratibu za chama hicho ili asikose sifa za kuteuliwa kupeperusha bendera ya CCM kwenye jimbo hilo ikiwa atashinda.
“Nawashukuru sana wana Iringa mnaonichangia fedha ili kuniwezesha kuchukua fomu, nathamini utu wenu nachowaomba mniombee,” alisema.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...