Meneja Bidhaa wa benki ya Exim, Bw Aloyse Maro akiokota moja ya kura za wateja wakati wa kuchezesha bahati nasibu ya kwanza ya kampeni ya akaunti ya malengo inayoendeshwa na benki hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.Wanaoshuhudia ni pamoja na mwakilishi wa Bodi ya michezo ya kubahatisha nchini Bw. Humudi Abdulhussein  (kushoto) na mmoja wa maafisa wa beki hiyo Bw George Musetti.

Benki ya Exim Tanzania imeendesha  droo yake ya kwanza ya kampeni ya akaunti ya malengo inayolenga kuhamasisha utamaduni wa kuweka akiba miongoni mwa watanzania.

Droo hiyo iliyosimamiwa na Bodi ya michezo ya kubahatisha nchini iliendeshwa mwishoni mwa wiki iliyopita jijini Dar es Salaam ikiwa ni droo ya kwanza kati ya sita zinazotarajiwa kuendeshwa katika kampeni hiyo.

Akizungumza mara tu baada ya droo hiyo, Meneja bidhaa wa benki hiyo, Bw. Aloyse Maro alisema kampeni hiyo ilizinduliwa ikiwa ni sehemu ya jitahada za benki hiyo kuwapatia wateja wake faida zaidi sambamba na huduma bora.

Alisema kwa kuanzia, washindi waliopatakina kupitia droo hiyo walifanikiwa kujitwalia zawadi za simu za kisasa aina ya iPhone 6 huku akitoa wito zaidi kwa wateja wa benki hiyo kuwa na mwitikio zaidi kwa kushiriki kwenye kampeni hiyo.

“Pamoja na kutoa shukrani zetu kwa wateja wetu kutokana na mafanikio tunayoendelea kuyapata ni vema pia tuwe mrejesho wa mafanikio haya  kwao pia. Ni katika mazingira hayo ndio maana tumekuwa na utaratibu wa kutoa zawadi kwa wateja wetu ili kufurahi nao pamoja,’’ alisema Bw. Maro.

 Zaidi Bw. Maro aliwakumbusha wateja wa benki kuendelea kushiriki zaidi kwenye kampeni hiyo kwa kuwa bado wananafasi zaidi ya kujishindia zawadi mbalimbali ikiwemo zawadi ya gari kwenye droo tano zilizosalia.

“Kampeni hii inaendelea kwa kipindi cha miezi mitano na bado kuna zawadi zaidi kwa ajili ya washiriki ikiwemo zawadi kuu ya gari ambayo itakabidhiwa kwa mshindi mwishoni mwa kampeni hii. Hivyo tunaomba watu waendelee kushiriki zaidi,’’ alisema.
 Sambamba na zawadi hizo Bw. Maro aliongeza kuwa kampeni hiyo inatoa riba nzuri zaidi kwa wateja wanaofungua akaunti hiyo ya malengo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...