Kama ambavyo aliweza kufanya vizuri na singo yake ya kwanza, msanii Galaxy anatarajia kuchomoka na wimbo wake mpya ‘mzuri tu’ ukiwa umeandaliwa na Man Walter chini ya studio za Combination sound hivi karibuni jijini Bongo.

The smart boy Galaxy Ikanda akiwa maejipanga fresh kwa ujio wake mpya, alielezea sababu zinazompelekea kutumia muda wake mwingi kujipanga na sio kukurupuka 

“Muziki umekuwa na ushindani mkubwa sana kiasi inampelekea msanii makini kuongeza umakini  na ubunifu kwenye utendaji Otherwise unaweza kujikuta kila siku umesimama sehemu moja huendi mbele, kitu ambacho sikitarajii kulingana na jitihada nilizonazo”.

Alisema “kinachoturudisha nyuma wasanii wengi ambao tunachipukia ni kutokuwa na nidhamu na kazi zetu wenyewa hata kwa wanaotusimamia (Managers), halikadhalika tuna pupa ya kutafuta shortcut kuyafikia mafanikio kirahisi bila kufanya juhudi, huku mi nasema ni kujidanganya”.

Galaxy ambaye kwa sasa yuko hewani na wimbo unaojulikana kwa jina la ‘Tam Tam’ amewataka wasanii wenzake kuongeza jitihata kwenye ubunifu na kuepuka kuzihusisha Sanaa zao na maisha yao binafsi ‘KUTENGENEZA KICKI’ kwa maana haiwasaidii na hii inachangia kuudidimiza muziki wetu na Sanaa kwa ujumla.

“sioni sababu ya msanii kutengeneza story ya uongo ili aweze kutoa wimbo wake, hii inaonesha dhahiri ni kutojiamini na sijawahi kuona imemsaidia msanii kwa kufanya hivyo wimbo ukapata umaarufu mwaka mzima, mara nyingi story za kutengeneza ili kutoa wimbo zikiisha na wimbo umeisha so zinaua muziki wetu kama vipi tukaze” – Galaxy. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...