
Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, akisalimiana na Mwandishi mwandamizi wa mtandao wa habari wa Modewjiblog, Andrew Chale alipotembelea katika banda la mtandao huo ambao mwaka huu mwezi Septemba unatimiza miaka 7 tangu kuanzishwa ambapo wametumia fursa ya maonyesho ya saba saba kukutana na wadau mbalimbali wanaotumia mtandao huo kupata habari mbalimbali sambamba na kubadilishana mawazo na ushauri wa maboresho ya kazi. Kushoto aliyefuatana naye ni Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu. Kulia ni mdau wa karibu na mshauri wa mtandao wa habari Modewjiblog, Lemmy Hipolite.

Mratibu Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa na mwakilishi wa Shirika la Maendeleo (UNDP) nchini, Alvaro Rodriguez, aliyeambatana na Mtaalam wa Mahusiano na Mawasiliano wa Umoja wa Mataifa (UN) Tanzania, Hoyce Temu akiangalia moja ya documentary ya TV katika banda hilo minayoonyesha wadau mbalimbali wanaotumia mtandao huu ambao walipata kuhojiwa.
Mmoja wa wadau wa Modewjiblog, Rehema Pascal akiuzungumzia mtandao wa habari wa Modewjiblog alipotembelewa ofisini kwake wakati wa kurekodi 'documentary' hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...