Mwigizaji wa filamu za vichekesho wa Kenya Benson Wanjau maarufu kama Mzee Ojwang (pichani) amefariki dunia Jumapili jioni katika hospitali ya Taifa ya  Kenyatta National alikokuwa amelazwa kwa matibabu. Taarifa kutoka NAirobi zinasema alikuwa anaumwa "Nimonia" (Pneumonia). 
Marehemu Mzee Ojwang alijipatia umaarufu mkubwa Afrika Mashariki kwa vituko vyake kwenye filamu za Vitimbi, Vioja Mahakami, Vituko na  Kinyonga. Alikuwa haonekani kwa muda mrefu kwenye televisheni za Kenya na mashabiki wake wakiwemo wa Tanzania walikuwa hawaishi kumuulizia aliko bila kupata jibu. 
Mola aiweke Mahali pema roho 
ya Mzee Ojwang - Amin.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 13, 2015

    R.I.P mzee Ojwang nilifurahia vichekesho vyako.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 13, 2015

    Rest in Peace Ojwang. Tutakukumbuka sana.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 13, 2015

    Poleni wafiwa huyu mzee ametuchekesha sana na mchezo wao na mama Kayai.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...