Askari Polisi kadhaa, mgambo na raia  wameuwawa kikatili na watu wanaosadikiwa kuwa ni majambazi waliovamia  kituo  cha Polisi cha Sitakishari, Ukonga,  jijini Dar es salaam usiku wa kuamkia leo. Silaha kadhaa pia inasemekana zimeporwa na majambazi hayo.
Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini IGP Ernest Mangu yupo eneo la tukio muda huu na ametangaza msako wa nguvu kuwasaka waliohusika na tukio hilo na kukomboa silaha zilizoporwa.

Kikosi kazi cha Globu ya Jamii kipo eneo la tukio kukusanya taarifa sahihi na rasmi kwa picha na video ambazo mtazipata baada ya muda si mrefu ujao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 13, 2015

    Mambo gani haya?

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 13, 2015

    Sio majambazi hawa watakua nu wale magaidi wanaovamia vituo vya polis

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 13, 2015

    JAMANI UZEMBE MWINGI NDANI YA JESHI LA POLISI, INTELIGENSIA YA WAZI (OPEN INTELLIGENCE) INAONYESHA WAZI KUWA VITUO VIDOGO VYA POLISI HASWA MAENEO YA MBALI NA MJI NA VYENYE ASKARI WACHACHE VIKO KATIKA HATARI/RISK YA KUVAMIWA HASWA USIKU. PIA ASKARI HAO HUWA WANALALA KAZINI NA HAWAKO MAKINI/ALERT KWAMBA LOLOTE LINAWEZA TOKEA SAA YEYOTE. POLISI KUWENI MAKINI NA WAELEVU MBELE YA UELEVU/AHEAD-OFF WA MAJAMBAZI. MAMBO YAMESHAHARIBIKA NCHINI - JOE BURA, DAR

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 13, 2015

    Hii inatisha na kusikitisha, ikiwa Polisi ndo tunaona sehemu salama Leo vituo vinavamiwa siye raia tutapona kweli?

    ReplyDelete
  5. Ni kweli polisi waongeze umakini zaidi

    ReplyDelete
  6. ukiona vituo vya polisi vinavamiwa na silaha kuibiwa basi jua kuna siku vita itatokea tz.. watu wanaiba na kujilinbikizia silaha tayari kwa vita..za kuambiwa changanya na za kwako-JMK

    ReplyDelete
  7. Raia tuwe na ushilikiano na vyombo vya ulinzi ilikutoa taarifa za watu wasio fahamika mapema

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...