Bendi maarufu ya muziki wa dansi Ngoma Africa Band aka FFU Ughaibuni yenye makao yake nchini Ujerumani, siku ya Jumapili 5 Julai 2015 ilitingisha jukwaa la Mamling Festival,liliofanyika kule Mining,Austria.
Kikosi kazi hicho cha Ngoma Africa band kilipangiwa kupanda jukwaani saa 10 na dakika 30 alasiri,lakini maporomota walisogeza muda hadi saa 12 jioni ndio bendi hiyo ilipopanda jukwaani,
Muda ulisogezwa kutoka na hali ya jua na joto kali lililofikia nyuzi joto 38c,ambazo sio za kawaida kwa msimu summer barani ulaya.
Kikosi kazi kilipopanda jukwaani bila ya kuremba remba walianza kuporomosha muziki moto moto kama kawaida yao,kiasi cha kuwafanya waandaaji watoe mwaliko tena kwa bendi hiyo kushiriki onyesho la 2016 Mungu akijalia.
Ngoma Africa baada ya kumaliza kazi wamerudi katika maskani yao ya himaya Anunnaki,kule Ujerumani
Ungana nao at www.facebook.com/ ngomaafricaband wasikilize at www.reverbnation.com/ ngomaafricaband
Ngoma Africa Band aka FFU Ughaibuni wakitesa katika tamasha la Mamling Festival, liliofanyika kule Mining,Austria.
Ras Makinja akiongoza gwaride la Ngoma Africa Band aka FFU Ughaibuni yenye makao yake nchini Ujerumani, siku ya Jumapili 5 Julai 2015 katika tamasha la Mamling Festival, liliofanyika kule Mining,Austria.
ffu-ughaibuni aka ngoma africa band bin watoto wa mbwa Big up guys
ReplyDeleteFFU wazee wa ubaya ubaya full gwaride NO kulala
ReplyDeleteNgoma Africa hongereni sana mnatisha mno, hard working guys
ReplyDeleteWATOTO WA MBWA BWAKENI ! KILA ANAYEPITA MBELE NG'ATA TAFUNA
ReplyDeleteFFU naona maafande kazini atakayeleta fujo atakiona cha mtema kuni
ReplyDeleteKaka Kamanda ras makunja naona chini ya ulinzi wa kikosi hatumwi mtoto hapo oh peleka ujumbe kwa kamanda
ReplyDelete