Wakazi wa Kijiji cha Kingwang’oko Tabora wapatiwa huduma za mawasiliano na Airtel WAKAZI wa Kijiji cha Kigwang’oko Wilaya ya Ulyankulu,wameipongeza kampuni ya Airtel kwa kuwajengea mnara wa mawasiliano na hivyo kuondokana na tatizo sugu la mawasiliano lililokuwa likiwakabili. 
 Wakazi hao wamekuwa wakifanya shughuli zao bila ya mawasiliano ya uhakika kwa muda mrefu jambo linalotajwa kukwamisha shughuli nyingi za maendeleo kijijini hapo. 
 Wanakijiji hao wameeleza kuwa, wamekuwa wakipata tabu ya kufanya mawasiliano wakati mwingine wakilazimika kupanda kwenye miti au vichuguu kupata mawasliano kabla ya kujengwa kwa mnara huo. 
 “Tunawashukuru sana Airtel kwa kutukumbuka na kutuleta mnara huu ambao hapa kijijini kwetu ni mkombozi mkubwa katika sekta ya mawasiliano” walisema wananchi hao Akiongea na waandishi wa habari mkazi wa Kigwang’oko, Juma Magema alisema 
“Kabla ya Airtel kuweka mnara hapa kijiji kwetu tulikuwa tunapanda katika miti na hata vichuguu ili kupata mawasiliano, lakini sasa hatupati tena shida hiyo” Akiuzindua mnara huo,aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua, John Kadutu, amewataka wananchi kuutumia mnara kuboresha shughuli zao za kijamii na kiuchumi na kuboresha maendeleo ya kijijini hapo na jamii kwa ujumla. 
 “Muutumie mnara huu kujiletea maendeleo kwani hivi sasa mnaweza kutumia mawasiliano ya Airtel na huduma zote zinazoenda sambamba na uwepo wa mnara huo kijijini hapo” alisema Kadutu 
 Awali meneja wa Airtel Mkoa wa Tabora,Fidelis Lugangira,alisema wamepeleka mnara huo ili kuboresha za kiuchumi ,lengo likiwa ni kuzidi kuwafanya wanufaike kwa kutumia mawasiliano. 
 “Mnara huu umejengwa kijijini hapa ikiwa ni hatua ya Kampuni yetu kusogeza karibu huduma za mawasiliano hivyo ni fursa ya kipekee kwenye kujiletea maendeleo” alisema Lugakingira. 
 Airtel imezindua huduma ya mawasiliano katika Kijiji cha Kigwang’oko Wilayani Ulyankulu mikoani Tabora mara baada ya kuzindua huduma kama hizo katika wilaya ya Ikungi mkoani Singida na katika kijiji cha Nduruma wilayani Arumeru mkoani Arusha. Mpango mkakati ni kufikia maeneo mengi zaidi husasani yaliyoko pembezoni mwa nchi
 Msimamizi wa Mnara wa Airtel Tabora, Bwana Phidelis Lugangila akimwonyesha sehemu za mnara , aliyekuwa Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua, John Kadutu baada ya uzinduzi wa mnara huo wa mawasiliano wa Airtel, utakaowawezesha wakazi wa kijiji cha
Kingwang’oko wilayani Uyankulu mkoani Tabora kupata mawasiliano bora. Akishuhudia ni Diwani wa kata ya Kona nne Bwana Japhael Lufungija akifatiwa na Afisa Masoko wa Airtel Tabora, Godfrey Kigata
 Picha ya pamoja baada ya uzinduzi wa mnara huo wa mawasiliano wa Airtel, utakaowawezesha wakazi wa kijiji cha Kingwang’oko wilayani Uyankulu mkoani Tabora kupata mawasiliano bora.
Wanannchi wakifurahia baada ya uzinduzi wa mnara huo wa mawasiliano wa Airtel, utakaowawezesha wakazi wa kijiji cha Kingwang’oko wilayani Uyankulu mkoani Tabora kupata mawasiliano bora.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...