Wanafunzi  wa Shule ya Msingi Kiseke Wilaya  ya Ilemela Mkoani Mwanza,  wakiwa wameketi kwenye madawati  64 yenye thamani  ya shilingi milioni 5 waliyokabidhiwa na Benki ya NMB kama sehemu ya msaada kwa shule hiyo.
Bw. Daniel Makorere, Afisa Elimu Wilaya ya Ilemela Mkoani Mwanza  akimshukuru Afisa Mkuu wa Fedha wa NMB Bw. Waziri Barnabas(kushoto) baada ya kupokea madawati yenye thamani ya shilingi milioni 5 kutoka benki ya NMB. Msaada huo wa madawati ulikabidhiwa kutoka NMB kwa Shule ya Msingi Kiseke ili kupunguza uhaba wa madawati unaoikumba shule hiyo. Wakishuhudia kutoka kulia ni Meneja wa NMB Kanda ya Ziwa Bw. Abraham Augustino pamoja na Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi Kiseke Bw, Denitrus Wima.
 Mkuu wa Wilaya  ya Busega Mkoani Mwanza Bw. Paulo Mzindakaya , akimpa mkono wa shukurani Afisa Mkuu wa Fedha wa NMB Bw. Waziri Barnabas(kulia), baada ya kukabidhi  madawati 240 yenye thamani ya shilingi milioni .... yaliyotolewa na benki ya NMB ukiwa ni msaada kwa  Shule za Msingi Nyashimo na Nasa Wilayani Busega pamoja na Sukuma na Simakitongo Wilaya ya Magu ili kupunguza uhaba wa madawati katika shule hizo. Kila shule imepata madawati sitini.
 Wanafunzi wa shule ya Msingi ya Kwibara wakiwa wameki kwenye madawati waliyokabidhiwa na NMB
Mkuu wa Wilaya  ya Musoma Mkoani Mara Bw. Zelothe Stephen , akimpa mkono wa shukurani Afisa Mkuu wa Fedha wa NMB Bw. Waziri Barnabas(kushoto), baada ya kukabidhi  madawati 330 yaliyotolewa na benki ya NMB ukiwa ni msaada kwa  Shule za Msingi Bwai, Kiriba, Chanyahuru na Busumi pamoja na shule ya Sekondari Kiriba zilizopo Musoma vijijini ili kupunguza uhaba wa madawati katika shule hizo. Kila shule imepata madawati hamsini na tano.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...