Ujumbe wa Mfuko wa GEPF nchini Tanzania na Mwenyekiti wa Watanzania waishio nchini Botswana wakiongozwa na Meneja Mahusiano wa Benki ya FNB Botswana, Bibi Patricia Mpelega (wa pili kushoto) wakati wakielekea kwenye tawi (Branch) la benki hiyo kwaajili ya uzinduzi wa akaunti maalum ya kuwasilisha michango kwa Watanzania wainshio nchini humo, kwa kujiwekea akiba zao za baadae.
Mkuu wa Kitengo cha Masoko kutoka Mfuko wa GEPF, Aloyce Ntukamazina (wa tatu kulia) akimpa maelezo mafupi juu ya mpango huo wa GDS Meneja Mahusiano wa Benki ya FNB Botswana, Patricia Mpelega, muda mfupi kabla ya kuzindua akaunti maalum.Wengine pichani ni Mwenyekiti wa watanzania waishio Botswana, Nieman Kissasi (kulia) na Meneja wa Mkoa wa Ilala Bw Jafari Meraji .
Bi Patricia Mpelega akimpongeza Mwenyekiti wa watanzania waishio Botswana, Nieman Kissasi baada ya kukamilisha zoezi la ufunguzi rasmi wa akaunti ya Diaspora Botswana
Mwenyekiti wa Watanzania waishio Botswana Bw Nieman Kissasi akikamilisha utaratibu wa kuwasilisha michango yake kama ishara ya uzinduzi rasmi wa akaunti hiyo kulia kwake ni Meneja wa Mkoa wa Ilala Bw Jafari Meraji .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...