Na Mwandishi Wetu 

“Suala la maadili si jipya, Watanzania watakumbuka tangu enzi la Azimio la Arusha misingi ya maadili imekuwa ikisisitizwa kama kijenzi muhimu cha ufanisi katika utoaji wa huduma kwa umma,” ni kauli ya Tixon Nzunda, Naibu Kamishna wa Maadili aliyoitoa siku ya uzinduzi wa Ahadi ya Uadilifu, Agosti 14, 2015, Ikulu Dar es Salaam. 

Kauli hii inasadifu ninachotaka kukieleza hapa katika makala haya na kwa hakika kumpa kongole Rais anayemaliza muda wake, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kwa kuamua kuhuisha suala la maadili kama kijenzi muhimu cha ufanisi katika utendaji wa sekta za umma na binafsi. 

Itakumbukwa kuwa Ijumaa iliyopita Reais Kikwete alizindua kile kinachoitwa Ahadi ya Uadilifu ambapo viongozi kadhaa wa umma na kutoka sekta binafsi walitia saini hadharani ahadi za kuendesha shughuli zao kimaadili zaidi. 

Ahadi ya Uadilifu kimsingi ni tamko rasmi na bayana la dhamira ya kuwa na mwenendo wa kimaadili na kuunga mkono Kampeni ya Kitaifa ya Maadili na Mapambano dhidi ya Rushwa. Kwa kusaini tamko hilo mhusika au taasisi inakuwa vimejipambanua kwa umma kuwa hawatajiingiza katika masuala yasiyo ya kimaadili katika utoaji wa huduma na uzalishaji.

Wazo la kuwa na Ahadi ya Uadilifu ni ubunifu kutoka maabara ya Mpango wa Matokeo Makubwa Sasa (BRN) iliyokuwa ikiangalia mbinu za kuboresha sekta ya mazingira ya biashara nchini. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...