Gabriel Ferdinand (kulia) mwanafunzi wa Musoma Mara
akikabidhiwa fedha na Meneja wa Airtel Musoma, Emmanuel Rafael
(Kushoto) baada ya kuibuka mshindi wa droo ya pili ya promosheni ya
“Jiongeze na Mshiko”.
Wakazi wawili wa Tabora na Musoma wameeleza furaha yao mara baada ya Kampuni ya mawasiliano ya Airtel kuendelea kukonga nyoyo za wateja wake na Watanzania kwa ujumla kwa kuwatangaza na kuwakabithi pesa zao baada ya kuibuka washindi wa wiki ya pili ya promosheni inayoendelea ya “Jiongeze na Mshiko”.

Washindi hao ni pamoja na , Gabriel Fernandis(18) mwanafunzi na mkazi wa wa Mkoa wa Musoma mkoani Mara, yeye amejishindi shilingi milioni 1 , na mshindi wa pili ni Hamis Rashid(52)na mkazi wa Sikonge mkoa waTabora yeye amejishindi shilingi milioni 3.

Sambamba na kukabithi zawadi hizo , Airtel imeendesha droo ya wiki ya tatu ya “Jiongeze na Mshiko” katika ofisi ya makao makuu ya kampuni ya Airtel iliyopo Morocco jijini Dar Es Salaam ilihudhuriwa na waandishi wa habari na wasimamizi kutoka bodi ya bahati nasibu Tanzania.

Akiongea mara baada ya kukabithiwa zawadi yake , Grabriel Fernandisi alisema”nimefurahi sana kuibuka mshindi katika promoshenii hii ambayo nimeshiriki bure , bila gharama yoyote na kujibu maswali na kujiongezea points zilizoniwezesha kushinda.

Nafurahia ushindi huu kwasababu pesa hizi zitanisaidia kujiendeleza kwenye masomo yangu” Akiongea na waandishi wa habari, Afisa uhusiano na matukio wa Airtel, Dangio Kaniki, amesema kwamba tunayofuraha kuwazawadia washindi wa wiki ya kwanza na ya pili ya promosheni “Jiongeze na Mshiko” ni matumaini yetu kuwa pesa hizi zitawawezesha kuendesha shughuli zao za kijamii na kiuchumi nakutatua changamoto mbalimbali wanazokumbana nazo.

Hamisi Rashid (kulia) mkulima wa Sikonge, Tabora akikabidhiwa
fedha na Meneja wa Airtel Tabora, Phidelis Lugangila (Kushoto) baada
ya kuibuka mshindi wa droo ya pili ya shindano la “Jiongeze na
Mshiko”.
Tutaendelea kuwazawadia wateja wetu kila wiki kwa muda wa wiki 16 hivyo natoa wito kwa watanzania kuendelea kujiunga na kushiriki katika promosheni hii bila gharama yoyote na kupata nafasi ya kujishindia.

Pamoja na kuwazawadia wateja wetu, leo pia tunaendesha droo ya wiki ya tatu na kutangaza washindi wengine wawili ambao wameibuka washindi. Katika droo ya leo tumebahatika kuwapata washindi wawili ambao ni pamoja na Afrillious Kapinaa (21) mwanafunzi, Mkazi wa Dar es Saalam amejishindia shilingi milioni moja pamoja na Shangai Rodger (53) mfanyakazi wa TRA na mkazi wa Tanga amejishindia shilingi milioni 3"

“Tunawashukuru wateja wetu na Watanzania wote walioshiriki na wenye sifa za kushiriki katika promosheni hii ya aina yake waendelee kushirikiIli kwa kutuma ujumbe wenye neno “BURE” kwenda namba 15470, na kisha kuanza kupokea maswali kwenye simu zao na kujibu maswali bure bila gharama yoyote na kujikusanyia pointi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...