* Wateja kupata Bonus ya mara tano zaidi kwa kununua muda wa maongezi
au kifurushi cha yatosha kupitia Airtel Money
* Wateja wote  wa malipo ya awali kufaidika


Kampuni ya simu za mikononi ya Airtel leo imezindua ofa kabambe kwa wateja wake wa Airtel Money ijulikanayo kwa jina la "Kamata tano Zaidi" itakayowawezesha wateja wa Airtel kupata muda wa maongezi mara 5 zaidi pindi watakaponunua muda wa maongezi au yatosha zaidi kupitia Airtel Money. 
 Akizungumza katika uzinduzi, Ofisa Mkuu wa Biashara wa Airtel , Arindam Chakrabarty alisema, kuanzishwa kwa bonus ya mara 5 zaidi kwa kununua muda wa maongezi kupitia Airtel Money ni katika juhudi za Airtel kuendeleza dhamira na azma yao ya kuwajali na kuwazawadia wateja . "Lengo letu ni kutoa huduma nafuu, zenye ubora, tija na zinazokidhi mahitaji ya mawasiliano kwa wateja wetu nchini kote. Nina imani "Kamata Tano Zaidi" italeta uhuru wa kuwawezesha wateja wetu kuwasiliana na familia zao,marafiki na hasa kuongeza ufanisi katika biashara zao popote pale walipo . " "Chakrabarty aliongeza kwa kusema, " tunawaahidi wateja wetu kupitia huduma ya Airtel Money tutaendelea kuwapa huduma za kisasa na kuwazawadia mara 5 ya matumizi yao kama bonus ya muda wa maongezi itakayowawezesha kupiga simu kwenda namba yoyote ya Airtel kwa siku hiyo". 
 Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mawasiliano wa AirtelTanzania, Beatrice Singano, alisema, "Bonus ya mara 5 zaidi itapatikana kwenye aina zote za manunuzi ya muda wa maongezi yatakayonunuliwa kwenye mfumo wa Airtel Money kwa kupiga *150*60# na kuchagua namba 2. Muda wa maongezi utakaonunuliwa utajumlisha muda wa maongezi wa kawaida pamoja na vifurushi vyote vya Yatosha au Yatosha Noma. Bonus ya mara 5 zaidi ya "Kamata Tano Zaidi" inayopatikana kwa kununua kupitia Airtel Money itadumu kwa muda wa masaa 24 toka muda uliponunuliwa, ili kuwatimizia wateja wetu mahitaji yao ya mawasiliano
Mkurugenzi  wa kitengo cha Mawasiliano wa Airtel Tanzania Beatrice Singano, akiongea  na waandishi wa habari wakati wa uzinduzi wa ofa ya "Kamata Tano Zaidi" inayowawezesha wateja wa Airtel kupata mara tano ya muda wa maongezi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...