MKURUGENZI
Mkuu wa Mfuko wa Fidia kwa Wafanyakazi, WCF, Masha Mshomba, akizungumza
kwenye mkutano na waandishi wa habari makao makuu ya Mfuko huo barabara
ya Bagamoyyo jijini Dar es Salaam, Agosti 16, 2015. Mfuko huo
ulioanzishwa kwa sheria ya bunge namba 20 kifungu cha 5 ya mwaka 2008,
una madhumuni ya kutoa fidia kwa Wafanyakazi kutokana na ulemavu au vifo
viinavyosababishwa na ajali au magonjwa yatokanayo na kazi sambamba na
kukuza mbinu za kuzuia matukio ya ajali, alisema. (Picha na K-VIS MEDIA)
Mfuko huo ambao umeanza kazi rasmi Julai 1, 2015, lengo kuu ni kutekeleza nia ya Serikali kukabiliana na changamoto za ulipaji wa fidia kwa Wafanyakazi katika mfumo wa utoaji fidia uliokuwepo awali, Mkurugenzi Mkuu Masha alizitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na kiwango kidogo cha malipo ya fidia(kiwango kisichozidi shilingi 180,000) kwa ulemavu wa kudumu na shilingi 83,000 kwa wategemezi endapo kifo kitatokea kwa Mfanyakazi husika. Akinukuu sheria iliyoanzisha Mfuko huo, Masha alisema, kifungu cha pili (2), cha sheria ya fidia kwa wafanyakazi namba 20/2008 Mfuko huu unawahusu Waajiri na Wafanyakazi wote katika sekta ya Umma na Binafsi, Tanzania Bara pekee. "Naomba ieleweke, anayepaswa kuchangia kwa mujibu wa sheria hii ni Mwajiri na sio Mfanyakazi kukatwa mshahara wake." Alifafanua Masha
Mfuko huo ambao umeanza kazi rasmi Julai 1, 2015, lengo kuu ni kutekeleza nia ya Serikali kukabiliana na changamoto za ulipaji wa fidia kwa Wafanyakazi katika mfumo wa utoaji fidia uliokuwepo awali, Mkurugenzi Mkuu Masha alizitaja changamoto hizo kuwa ni pamoja na kiwango kidogo cha malipo ya fidia(kiwango kisichozidi shilingi 180,000) kwa ulemavu wa kudumu na shilingi 83,000 kwa wategemezi endapo kifo kitatokea kwa Mfanyakazi husika. Akinukuu sheria iliyoanzisha Mfuko huo, Masha alisema, kifungu cha pili (2), cha sheria ya fidia kwa wafanyakazi namba 20/2008 Mfuko huu unawahusu Waajiri na Wafanyakazi wote katika sekta ya Umma na Binafsi, Tanzania Bara pekee. "Naomba ieleweke, anayepaswa kuchangia kwa mujibu wa sheria hii ni Mwajiri na sio Mfanyakazi kukatwa mshahara wake." Alifafanua Masha
Waandishi wa Habari kazini
Masha
(katikati), akiwa na Kaimu Mkurugenzi wa hifadhi za Jamii kutoka Wizara
ya Kazi na Ajira, Daudi Kaali, (kulia) na Mkurugenzi wa Utafiti,
Tathmini na Sera wa Mamlaka ya Kusimamia Mifuko ya Hifadhi ya Jamii
Nchini, SSRA, Ansgar Mushi.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
shida ni kuzipata hizo hela za fidia pale unapokumbwa na matatizo yanahitaiji ulipwe fidia
ReplyDelete