BARAZA la Sanaa la Taifa (Basata) limeipongeza kampuni ya Compass Communications Tanzania kwa kufanya mashindano bora ya Miss Universe hapa nchini.

Kauli hiyo imetolewa na  Mratibu wa mashindano ya Miss Universe Fausta Magoti wakati wa kufanya tathimini ya mashindano ya mwaka jana ambapo, Caroline Benard aliibuka mshindi.

Magoti alisema kuwa pamoja na kampuni ya Compass kuanza kushiriki katika mashindano ya Miss Universe mwaka 2007, waliweza kufanya vyema na kuitangaza Tanzania nje ya mipaka yake.

Mbali ya kufanya vizuri katika mashindano ya kimataifa, Magoti alisema kuwa wameridhishwa sana na utendaji wa kamati hiyo kwa kuteua majaji ambao wamekuwa wakiwatangaza washindi ambao ni mfano bora kwa tabia kwa jamii.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...