Kamanda Mpinga,
akishiriki dua ya pamoja na wachezaji wa timu ya Kamati ya Amani ya Viongozi wa
Dini, baada ya mazoezi yao timu hiyo yanayoendelea kwenye Uwanja wa Karume
jijini Dar es Salaam, kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa kirafiki na timu ya
Kamati ya Amani ya Mkoa wa Arusha unaotarajia kuchezwa mwezi ujao jijini Arusha
na ule wa kirafiki kati yao na timu ya Mabalozi hivi karibuni. Kamanda Mpinga
alifika kuwatembelea wachezaji hao kujionea maendeleo ya mazoezi yao.
Kamanda Mpiga akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu ya Kamati ya Amani ya Viongozi wa Dini ya Mkoa wa Dar es Salaam,baada ya mazoezi ya timu hiyo yaliyofanyika leo asubuhi kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam. Kamanda Mpinga alifika kuwatembelea wachezaji hao kujionea maendeleo ya mazoezi yao.
Kamanda Mpinga, akisalimiana na walimu wa timu hiyo, baada ya mazoezi yao kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam, leo asubuhi.
Picha ma www.sufianimafoto.com
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...