Mgombea Urais wa CCM,Dkt John Pombe Mgufuli akiweka shada la Maua kwenye kaburi la Marehemu Kapteni Komba aliyezikwa kijijini kwao Lituhi mkoani Ruvuma.
Mgombea
Urais wa CCM Dkt John Pombe Magufuli akiwasalimia wananchi wa Songea
waliokuwa wamefurika kwenye uwanja wa Maji Maji mjini humo mkoani
Ruvuma,Mgombea huyo ambaye anawaomba Watanzania ridhaa ya kuwaongoza
katika awamu ya tano,amewaambia kuwa katika serikali yake wakulima hawatokopwa mazao yao, mbolea zitapatikana kwa wakati, barabara zitaboreshwa ,elimu bure mpaka kidato cha nne, kuongeza maslahi ya walimu pamoja na kuboresha huduma za afya.
Mgombea
wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM)Dk. John Pombe Magufuli
akihutubia umati wa wakazi wa mji wa Songea, ambapo alisema katika
serikali yake wakulima hawatokopwa mazao yao, mbolea zitapatikana kwa
wakati, barabara zitaboreshwa ,elimu bure mpaka kidato cha nne, kuongeza
maslahi ya walimu pamoja na kuboresha huduma za afya.
Mgombea Ubunge Jimbo la Peramiho, Jenista Mhagama akipokea Ilani ya Uchaguzi ya CCM kutoka kwa Mgombea Urais kupitia chama hicho, Dk Magufuli wakati wa mkutano huo wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Tamasha mkoani Ruvuma.
Dk Magufuli akimnadi Mgombea Ubunge wa CCM Jimbo la Nyasa, Stelah Manyanya katika mkutano wa kampeni katika Mji wa Lituhi,ambapo pia alimkabidhi Ilani ya chama hicho.
Mgombea wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM)Dk. John Pombe Magufuli akimkabidhi mgombea ubunge wa Jimbo la Mbinga Ndugu Sixtus Mapunda kitabu cha Ilani ya Uchaguzi ya CCM kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Mbinga mjini.
Dk Magufuli akishuka kwenye Kivuko cha Mto Ruhuhu akitokea Wilaya ya Ludewa Mkoani Njombe kwenda Mbinga mkoani Ruvuma kuendelea na kampeni za urais ubunge na udiwani. Dk Magufuli ameahidi kujenga daraja la mto huo.
Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM,Dkt John Pombe Magufuli akizungumza jambo na mkazi wa mji wa Peramiho ambaye ni mlemavu wa ngozi,jioni ya leo mara baada ya kumaliza kuwahutubia wananchi wa mji huo kwenye mkutano wa hadhara wa kampeni.
Dk Magufuli akimsalimia mmoja wa walemavu waliojitokeza kwenye mkutano wa kampeni mjini Mbinga.
Mjumbe wa Kamati Kuu ya CCm Dk. Emmanuel Nchimbi akihutubia wakazi wa Songea mjini ambapo aliwataka wananchi hao kumpa kura nyingi Mgombea wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM)Dk. John Pombe Magufuli kwenye uchaguzi utakaofanyika Oktoba 25,kwa sababu ni Muaminifu,muadilifu na ni mchapa kazi.
Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi ambaye pia ni mjumbe wa Kamati Kuu ya CCM Taifa Ndugu William Lukuvi akihutubia wakazi wa Songea mjini kwenye mkutano wa kampeni za CCM uliofanyika kwenye uwanja wa Maji Maji jioni ya leo.
Maelfu
ya Wananchi wakiwa wamefurika ndani ya uwanja wa maji maji mjini Songea
jioi ya leo kwenye mkutano wa kampeni wa CCM,mkoani Ruvuma jioni ya
leo,ambapo Mgombea Urais wa CCM Dkt John Pombe aliwahutubia wananchi
hao.
Ushindi unakuja.
ReplyDelete