Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Prof Mkenda  Akiwa na Mwenyekiti na Afisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam life Insurance Ndg.Julius Magabe Tayari kwa Uzinduzi wa  Kampuni ya Sanlan. 
Mgeni rasmi Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha Prof Mkenda wa Pili Kushoto Akiwa na Mwenyekiti na Afisa Mtendaji Mkuu wa Sanlam life Insurance Ndg.Julius Magabe, wa pili kulia Pamoja na 
Mtendaji Mkuu wa umoja wa makampuni ya Sanlam.Ndugu.Ian Kirk..Israel Kamuzora, Kamishna wa Bima katika Mamlaka ya Bima Tanzania (TIRA) Mara baada Uzinduzi wa wa Kampuni ya Sanlan wakionyesha Mshikamano.Kampuni inayoongoza katika bima za maisha nchini, African life .

Assurance(Aflife) jana usiku wa Agosti 12, 2015 ilitangaza rasmi Kubadilisha jina lake la kibiashara na kuwa Sanlam Life Insurance ambayo ni Kampuni ya kimataifa ya huduma za kifedha yenye makao yake makuu Afrika ya Kusini, ambayo imekuwa na umiliki mkubwa zaidi wa hisa za kampuni hiyo tangu mwaka 2005.Badiliko hili ni kwa mujibu wa umoja wa makampuni ya Sanlam yenye lengo la kupanua wigo na kuimarisha uwepo wake nchini TanzanianaAfrika Mashariki kwa ujumla.Kwa upande wa wateja, wanahisa, mawakala na wafanyakazi, badiliko hili kuwa Sanlam Life Insurance litaimarisha faida za ushirika zilizojengwa kwa miaka 10 sasa.

Kwa mujibu wa Bw Magabe, Sanlam Group ni kampuni ya kuheshimiwa Afrika yenye matawi katika nchi 12. "Kwenye suala la wateja kuridhika na uaminifu, Sanlam imekuwa ikiipa sekta ya bima ya maisha kipaumbele kwa wakazi wa Afrika Kusini. 

Vile vile, kwa Tanzania Aflife daima imekuwa ikisifika kwa kuwa na huduma bora kwa wateja na kupewa alama za AA-na kampuni ya viwango ulimwenguni ya Global Credit Rating (GCR) kwa nguvu ya kifedha na ulipaji bora wa madai.”mabadiliko kutoka Aflife kuwa Sanlam Life Insurance yatachangia utendaji wa kibiashara kwa kampuni. "Kuna mipango ya kupanua soko la rejareja na kutoa huduma za ziada zilizo endelevu katika ukuzaji wa biashara, wateja wa Sanlam Life Insurance watapata bidhaa mpya zilizoboreshwa zaidi.”

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...