Na  Bashir  Yakub

Hapa  kwetu  Tanzania  tunazo  ndoa za  aina  kuu  mbili. Kwanza  tunazo  ndoa  za  kiraia au  kiserikali, na  pili  tunazo  ndoa  za  kimila. 

Ndoa  za  kiraia  au  za  kiserikali   kama  zinavyojulikana kwa  wengi  ni  zile  ambazo  hufungwa chini  ya  usimamizi  wa  mamlaka  za serikali  kama  ofisi  ya  mkuu  wa  wilaya n.k.  Na  kwa upande  wa  ndoa za kimila    hizi  ni  zile  ambazo  hufungwa  kutokana  na  taratibu  za  watu  wa  kabila  au  koo  fulani  kwa  mujibu wa  tamaduni  na desturi  zao.  Ndoa  za  kimila  hujumuisha  pia ndoa  zinazofungwa  kwa  taratibu  za  kidini.

 Kwa  taratibu  za kidini  tunapata ndoa  nyingi  kwa  mfano  ndoa  zinazofungwa  kwa  mujibu  wa  mafundisho  ya  kiislam,  ndoa  zinazofungwa  kwa mafundisho  ya  kikristo,  budha , wahindu   na  dini  nyingine pia wanazo  taratibu  zao. 

Aidha  sehemu  za  kufungia ndoa  kisheria  ni  maeneo  ya nyumba  za  ibada, kwenye ofisi  za  serikali,  ubalozini  kwa  walio  nje  ya  nchi,  majumbani  na  sehemu  nyingine  ambazo  ni  wazi  kwa  watu  kushuhudia. Pamoja  na  hayo  yote  juu  yafaa  tujue  kuwa  zipo  aina  za  ndoa  au  mahusiano  yaliyokatazwa kabisa  kuitwa  ndoa. 

Juu  ya  hilo  sheria  imeainisha  mambo  ambayo  yakifanywa  au  yakipitiwa  ndoa  inakuwa  halali halikadhalika yale  ambayo   yakifanywa  au  kutofanywa  ndoa  inakuwa  haramu.Haya  ni  mengi  isipokuwa hapa  tutaona  baadhi  yake. Pamoja  na  hayo  kabla  ya kuyaona hayo kwanza  tuangalie  baadhi  ya  taratibu  za kupitia  kabla  ya  kuendea  suala  la  kufunga  ndoa.

1.BAADHI  YA  MAMBO  YA  KUZINGATIA  WAKATI  WA  KUFUNGA  NDOA.
( a ) Kifungu  cha  28  cha  sheria  ya  ndoa  kinasema  kuwa  ikiwa  ndoa  itafungwa  katika  ofisi  za   wilaya,  kwenye  nyumba   za  ibada  au  popote  kwenye    jamii  basi  ni  vema  ikawa  ruhusa kwa   wanajamii  au   waumini  wa  nyumba  hiyo  ya  ibada  kushuhudia   bila  kuzuiwa.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...