Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla (kulia), akisalimiana na Afisa Ugavi Mkuu wa Bohari Kuu ya Maji, Datus Bahati mara baada ya kuwasili Bohari Kuu ya Maji wakati wa ziara yake ya siku tatu ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maji katika mkoa wa Dar es Salaam inayosimamiwa na Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka mkoa wa Dar es Salaam (DAWASA) ambapo aliitimisha ziara hiyo Agosti 27, 2015 kwakukagua miradi iliyopo daraja la mpiji na Kerege na maungio ya maji ya wazo.
Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla (katikati) akipata maelezo kutoka kwa Bohari Mkuu wa Wizara ya Maji, Crepn Balamu, jinsi mita za kisasa kutoka Uturuk zinavyofanya kazi ambapo amesema kazi yao ni kuingiza na kuwauzia mamlaka za maji katika miji nchini, kushoto ni Kaimu Mtendaji Mkuu wa Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka (DAWASA), Mary Mtukula.
Kutoka kulia ni Bohari Mkuu wa Wizara ya Maji, Crepn Balamu akimpa maelezo Naibu Waziri wa Maji, Amos Makalla vifaa vya kuunganisha maji wakati wa ziara yake ya siku ya kukagua utekelezaji wa miradi ya maji katika mkoa wa Dar es Salaam inayosimamiwa na Mamlaka ya Maji Safi na Maji Taka mkoa wa Dar es Salaam (DAWASA)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...