Na Grace Michael

Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya umekutana na Uongozi wa Mamlaka ya Vitambulisho (NIDA) kwa lengo la kubadilishana uzoefu na changamoto katika suala la utambuzi wa watumiaji wa huduma za vitambulisho.

Hatua hiyo ya NHIF kukutana na uongozi huo inakusudia kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wanachama wake ambao tayari wana vitambulisho vya Taifa.

Akizungumzia hatua hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa NHIF Bw. Michael Mhando, amesema Mfuko wake umeona kuna umuhimu mkubwa wa kuunganisha nguvu na rasilimali chache zilizopo katika eneo hilo kwa manufaa ya wote.

“Tumeona ni vyema tutakakutana na wenzetu wa NIDA ili kuona ni kwa namna gani tunaweza kurahisisha upatikanaji wa huduma kwa wanachama wetu kupitia vitambulisho vya Taifa lakini pia kubadilishana uzoefu katika uandaaji wa vitambulisho ambavyo ni vya kisasa zaidi,” alisema.

Naye Mkurugenzi wa Mifumo Habari wa NHIF, Bw. Ali Othman amesema kuwa hatua hiyo ni fursa kubwa kutokana na ukweli kwamba kitambulisho cha Taifav kitamuwezesha mwananchi kutumia huduma mbalimbali.

“Kitambulisho cha Taifa kinajibu nani ni nani, anakaa wapi, anamiliki nini na anafanya nini taarifa ambazo ni za muhimu sana katika kuuwezesha Mfuko kutambua kila kundi na namna ya kuhamasisha kuwa na Mfumo wa bima ya afya kulingana na kundi husika,” anasema.

Ametumia mwanya huo kuushukuru uongozi wa NIDA KWA KUUSHIRIKISHA Mfuko katika hatua za awali za uandaaji na ubunifu wa vitambulisho vya Taifa jambo ambalo litarahisisha sana utekelezaji wa hatua hii ya sasa.

Bw. Othman amesema kuwa kwa kutumia teknolojia ya Mifumo Habari kuna uwezekano mkubwa wa wanachama wa NHIF kutumia vitambulisho vya Taifa sanjari na NHIF katika upatikanaji wa huduma ikiwemo udhibiti wa mianya ya udanganyifu hivyo Mfuko unatarajia kwa kila hali kuanza kutumia vitambulisho vya NIDA katika utambuzi wa wanachama wake.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...