Na Lorietha Laurence-Maelezo

Bodi ya Mfuko wa Barabara nchini(RFB) imefanikiwa kufanya maboresho ya barabara kwa kiwango cha lami katika kipindi cha miaka kumi ya uongozi wa Serikali ya awamu ya nne wa Mhe. Jakaya Kikwete.

Akizungumza na waandishi wa habari Dar es Salaam Jana Bw. Joseph Haule amesema kuwa matengenezo hayo yamefanikisha ujenzi wa barabara kuu zinazounganisha mikoa mbalimbali nchini kukamilika kwa asilimia 89 huku zile za Wilaya na Miji kwa asilimia 57.

“ kazi kubwa ya Mfuko huu ni kukusanya mapato kupitia vyanzo mbalimbali ikiwemo tozo za barabarani na ushuru wa mafuta na baadaye kuzigawa kupitia taasisi zinazohusika na ujenzi wa barabara ikiwemo TANROADS, Wizara ya Ujenzi na Ofisi ya Waziri Mkuu “ alisema Bw. Haule

Aidha aliongeza kuwa Mfuko huo umefanikisha ujenzi wa daraja la Mabatini jijini Mwanza ,daraja la Mwanhunzi na daraja la Mbutu linalounganisha Igunga na Shinyanga pamoja na ununuzi wa vivuko kikiwemo kile cha Mv Malagarasi.

Mbali na hayo Bw.Haule aliongeza kuwa Bodi hiyo inaendelea kuhakikisha barabara zinatunzwa kwa kudhibiti magari ya mizigo yanayozidisha uzito unaochangia uharibifu wa barabara kwa kuanzisha mfumo wa kisasa wa kamera utakaokuwa unaratibiwa na mfuko huo.

Mfuko huo umefanikiwa kuanzisha ujenzi wa barabara kwa kutumia mawe ambao ni wa gharama nafuu na wa kudumu kwa muda mrefu,hata hivyo miradi hiyo imeanza kutekeleza katika mikoa ya Kigoma na Mwanza.

Kutokana na mtandao wa barabara kufanyiwa matengenezo ya mara kwa mara imesaidia kuongeza ubora wa barabara na kupanua wigo wa biashara kati ya Tanzania na nchi za jirani ikiwemo Zambia,Malawi,Burundi,Rwanda na Uganda.

Mbali na mafanikio hayo Mfuko huounakabiliana na changamoto mbalimbali ikiwemo upungufu wa bajeti kutokana na fedha zinazopatikana kutokukidhi mahitaji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Kazi nzuri mwenye macho aambiwi tazama

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...