Kaimu Katibu Mkuu, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw. HAB Mkwizu anasikitika kutangaza kifo cha Bw. Boniphace Haule - Mhasibu Mkuu wa Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma (Pichani) kilichotokea nchini India tarehe 10.08.2015.
Mwili wa Marehemu utawasili leo, uwanja wa ndege wa J.K. Nyerere. Mazishi yatafanyika Ijumaa tarehe 14/08/2015. Msiba uko nyumbani kwa marehemu Tegeta Ununio, Mtaa wa Mwaitende.
Maziko yanatarajia kufanyika katika makaburi ya KINONDONI.
Taarifa na taratibu za msiba zitafuata.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...