indexG
MUIMBAJI mahiri wa muziki wa Injili anayetamba katika muziki huo, Upendo Nkone amekubali kushiriki katika Tamasha la Kuombea amani katika uchaguzi Mkuu unaotarajia kufanyika Oktoba 25 mwaka huu.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama Nkone ni muimbaji wa kwanza wa Tanzania kukubali kushiriki katika tamasha la hilo la Amani linalotarajia kufanyika Oktoba 4.
Msama alisema  wanaendelea na mchakato wa kuzungumza na waimbaji wengine ili kuwa na idadi kubwa ya waimbaji wa Tanzania sambamba na wengine kutoka nje.
Msama alisema wanajipanga kualika waimbaji kutoka nchi tano za Afrika kwa lengo la kunogesha uzinduzi huo ili ujumbe wa neno la Mungu ufike kwa dhati.Aidha Msama alisema sambamba na waimbaji kutoka nje ya Tanzania pia wanajipanga kutangaza amani katika mikoa 10 ya Tanzania bara.
“Tunaendelea na mikakati ya kufanikisha Tamasha hilo ambalo litakuwa ni la aina yake, hivyo wadau mbalimbali wasubiri tamasha hilo,” alisema Msama.
Msama alisema Tamasha hilo litahudhuriwa na wadau mbalimbali kwa kushirikisha wanasiasa, viongozi wa dini mbalimbali na makundi mengine kama wasanii na wanamichezo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...