JESHI  la Polisi  Kanda Maalum ya Dar es Salaam linatarajia kuzindua mashindano ya michezo mbalimbali kwa lengo la kuwashirikisha wananchi  wa  rika zote  na  itikadi  mbalimbali 
yatakayojulikana“KAMISHNA KOVA CUP”.

 Madhumini ya mashindano haya ni  ni  Kuwaunganisha wananchi wenye itikadi mbalimbali ili kupitia mashindano  haya  watakaoshiriki  watajifunza  masuala  ya usalama, uzalendo  na kuzingatia utaifa kwa madhumuni ya kuwashirikisha kikamilifu katika ulinzi wa nchi na kudumisha amani  na  utulivu  katika  jiji  la  Dar  es  Salaam  na  mikoa mingine.

Lengo lingine ni  Kuishirikisha jamii  kuondokana na dhana ya kutenda uhalifu wa aina mbalimbali kama vile ujambazi, matumizi ya aina mbalimbali ya  madawa ya kulevya,  wizi katika mitandao,uzururaji, na kukaa katika vijiwe bila kazi.

Pia  Kupitia michezo mbalimbali, jamii itafaidika kupata elimu juu ya umuhimu wa jukumu la msingi la kushiriki katika ulinzi na usalama  wa  nchi  hii,  itakuwa  ni  fursa  nzuri  kujua madhara ya kujihusisha na vitendo vya uhalifu.

Katika michezo watajifunza kujenga au kuimarisha mahusiano mema baina ya Jeshi la Polisi na  jamii  kwa  ujumla  kupitia  dhana  ya  Polisi  Jamii itatekelezwa kwa vitendo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...