Viongozi waandamizi wa Tanzania Bloggers Network (TBN) wakigonganisha glasi na Afisa Mahusiano ya Umma wa Ubalozi wa Marekani Bi. Marissa Maurer (wa tatu kushoto) na Afisa wa Siasa na Uchumi wa ubalozi huo Bw. Vincent Spera (wa pili kushoto) walipokutana jijini Dar es salaam kwa mazungumzo yasiyo rasmi ili kubadilishana mawazo ya njia bora ya kuendeleza tasnia hiyo ya habari za mtandao inayokuja juu kwa kasi nchini. 
TBN ni umoja wa bloggers wapatao 100 waliouunda ili kujiendeleza na kusimamia maslahi yao huku wakisaidia kusukuma mbele gurudumu la maendeleo ya Taifa nay a tasnia ya habari kwa jumla. Wengine toka kulia ni wajumbe wa TBN Max Mello, Joachim Mushi (Mwenyekiti), Monica Mara (Afisa Mipango), Hadija Kalili  (Katibu), Shamim Mwasha (mtunza hazina) na Afisa habari wa ubalozi huo Japhet Sanga. Picha kwa hisani ya TBN

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...