Kampuni ya mawasiliano ya Vodacom imekanusha taarifa za uvumi zilizotangazwa na baadhi ya vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kuwa inaendesha kampeni kupitia ujumbe mfupi wa maneno kumfanyia kampeni mgombea urais kupitia UKAWA.

Vyombo hivyo viliandika habari za uzushi kuwa Vodacom imeanzisha promosheni kupitia ujumbe mfupi wa maneno inayojulikana kama “Jiunge na Lowassa” kitu ambacho hakipo.

Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania,Rene Meza ameeleza kuwa kampeni zinazoendeshwa hivi sasa na Vodacom zinahusiana na kuwaongezea muda wa maongezi na data wateja wake na haina kampeni nyingine yoyote.

“Katika siku za karibuni tulizindua kampeni kwa ajili ya wateja wetu zinazohusiana na kuwapatia wateja wetu ofa ya muda wa maongezi na data hatuna kampeni zozote za kisiasa  wala hatujihusishi na kampeni za vyama vya siasa bali tupo kwa ajili ya kuwahudumia watanzania wote na kuendelea kutoa huduma bora za mawasiliano nchini kote”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...