Na Woinde Shizza,Arusha
Jiji la Arusha limeendelea kuwa kinara katika mchezo wa tenisi baada ya wachezaji wake kuibuka kidedea kwa kutwaa ushindi katika umri tofauti tofauti ,mashindano yaliyomalizika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya Arusha Tenisi gymkhana klabu.

Mashindano hayo yalidhaminiwa na Jubilee tyres ikiwa ni mwaka wa tatu sasa, yalishirikisha jumla ya wachezaji 90 ambao 28 kati yao ni wasichana kutoka Dar es salaam gymkhana klabu,Kijitonyama tenisi klabu kutoka Dar es salaam,Morogoro tenisi klabu, ISM –Moshi campus, AICC klabu –Arusha pamoja na Arusha tenis gymkhana klabu.

Katika umri wa miaka 6 kwa wasichana Schaefer Swantje kutoka ISM Moshi campus alifuatiwa na Suhana  Patel kutoka Arusha gymkhana klabu,huku kwa  upande wa wavulana wa umri huo Sahil Shah kutoka ISM moshi campus na kufuatiwa na Yuvraj Sidhu kutoka Arusha gymkhana klabu.
Kusoma zaidi bofya HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...