Na Woinde Shizza,Arusha
Jiji la Arusha limeendelea kuwa kinara katika mchezo wa
tenisi baada ya wachezaji wake kuibuka kidedea kwa kutwaa ushindi katika umri
tofauti tofauti ,mashindano yaliyomalizika mwishoni mwa wiki katika viwanja vya
Arusha Tenisi gymkhana klabu.
Mashindano hayo yalidhaminiwa na Jubilee tyres ikiwa ni
mwaka wa tatu sasa, yalishirikisha jumla ya wachezaji 90 ambao 28 kati yao ni
wasichana kutoka Dar es salaam gymkhana klabu,Kijitonyama tenisi klabu kutoka
Dar es salaam,Morogoro tenisi klabu, ISM –Moshi campus, AICC klabu –Arusha
pamoja na Arusha tenis gymkhana klabu.
Katika umri wa miaka 6 kwa wasichana Schaefer Swantje kutoka
ISM Moshi campus alifuatiwa na Suhana
Patel kutoka Arusha gymkhana klabu,huku kwa upande wa wavulana wa umri huo Sahil Shah
kutoka ISM moshi campus na kufuatiwa na Yuvraj Sidhu kutoka Arusha gymkhana
klabu.
Kusoma zaidi bofya HAPA
Kusoma zaidi bofya HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...