Meneja
wa benki ya Exim Tanzania tawi la Mbeya, Bw Iddy Mwacha(kushoto)
akikabidhi msaada wa vitabu vya masomo kwa mmoja wa wanafunzi
aliewawakilisha wanafunzi wenzie na uongozi wa shule ya sekondari Sinde
iliyopo eneo la Mwanjelwa mkoani Mbeya katika kupokea msaada huo ikiwa
ni mwendelezo wa harakati za benki hiyo katika kuisadia serikali
kuboresha hali elimu na ufaulu wa wanafunzi hapa nchini. Wanaoshuhudia
ni baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo, uongozi wa shule pamoja na
wanafunzi.

BENKI ya Exim Tanzania imetoa msaada wa vitabu vya masomo vyenye thamani ya sh mil. 8/- kwa shule ya sekondari Sinde iliyopo eneo la Mwanjelwa mkoani Mbeya ikiwa ni mwendelezo wa harakati za benki hiyo katika kuisadia serikali kuboresha hali elimu na ufaulu wa wanafunzi hapa nchini.
Akizungumza kwenye hafla fupi ya makabidhiano ya vitabu hivyo iliyofanyika kwenye viunga vya shule hiyo mwishoni mwa juma lililopita, Meneja wa benki hiyo tawi la Mbeya Bw Iddy Mwacha alisema msaada huo ni sehemu ya uthibitisho wa namna benki hiyo imekuwa ikipambana kuhakikisha uwepo wake hapa nchini unaleta tija zaidi kwa jamii.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...