Meneja wa benki ya Exim Tanzania tawi la Mbeya, Bw Iddy Mwacha(kushoto) akikabidhi msaada wa vitabu vya masomo kwa mmoja wa wanafunzi aliewawakilisha wanafunzi wenzie na uongozi wa shule ya sekondari Sinde iliyopo eneo la Mwanjelwa mkoani Mbeya katika kupokea msaada huo ikiwa ni mwendelezo wa harakati za benki hiyo katika kuisadia serikali kuboresha hali elimu na ufaulu wa wanafunzi hapa nchini. Wanaoshuhudia ni baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo, uongozi wa shule pamoja na wanafunzi.
BENKI ya Exim Tanzania imetoa msaada wa vitabu vya masomo vyenye thamani ya sh mil. 8/- kwa shule ya sekondari Sinde iliyopo eneo la Mwanjelwa mkoani Mbeya ikiwa ni mwendelezo wa harakati za benki hiyo katika kuisadia serikali kuboresha hali elimu na ufaulu wa wanafunzi hapa nchini.
Akizungumza kwenye hafla fupi ya makabidhiano ya vitabu hivyo iliyofanyika kwenye viunga vya shule hiyo mwishoni mwa juma lililopita, Meneja wa benki hiyo tawi la Mbeya Bw Iddy Mwacha alisema msaada huo ni sehemu ya uthibitisho wa namna benki hiyo imekuwa ikipambana kuhakikisha uwepo wake hapa nchini unaleta tija zaidi kwa jamii.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...