D3A_5097
Mkurugenzi M-Net Kanda ya Afrika Magharibi, Wangi Mba-Uzoukwu akifafanua jambo kwa waandishi wa habari (hawapo pichani) kutoka nchi za Afrika waliokusanyika kwenye jukwaa kubwa la kuonesha vitu mbalimbali vinavyoburudisha katika chaneli za DStv na GoTv kupitia MultiChoice hivi karibuni nchini Mauritius.
D3A_5116
Mkurugenzi wa M-Net kwa nchi za Afrika Mashariki na SADC, Theo Erasmus akifurahi jambo kwenye mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) kutoka nchi mbalimbali za Afrika.

Na Modewjiblog, Mauritius
Moja ya makampuni yanayoongoza katika utoaji wa vipindi vya burudani barani Afrika M-Net imesema kwamba itazindua chaneli maalumu kwa ajiri ya wakazi wa Tanzania itakayojulikana kama maisha Magic Bongo.
MAISHA MAGIC BONGO itaruka hewani kupitia chaneli 160 ya DStv kuanzia Alhamisi ya Oktoba Mosi mwaka huu na itapatikana katika vifurushi vyote vya Access, Family, Compact, Compact Plus na Premium.

Imeelezwa kuwa ingawa mambo yametengenezwa mahsusi kwa ajili ya Watanzania mataifa jirani yaAfrika Mashariki ikiwamo Kenya, Uganda, Ethiopia na DRC wanaweza kuona.

Uamuzi huo wa M-Net umefanyika wakati mchakato unaendelea wa kuboresha zaidi ulaji kwa wateja wake.

Hata hivyo wamesema kwamba MAISHA MAGIC EAST ambayo kwa sasa inaruka kupitia chaneli 158 itajiimarisha zaidi katika soko la Kenya huku ikiendelea na mara moja kwa wiki kwa ajili ya soko la Uganda ndani ya Luganda.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...