Msajili  Msaidizi wa ofisi ya msajili  wa Vyama  vya Siasa, Sisty Nyahoza akizungumza na waandishi wa habari hawapo pichani juu ya kuufahamisha umma kuwa chama cha siasa Tanzania Peoples Party (TPP) kilifutwa kwenye orodha ya vyama vya siasa hapa nchini na chama hicho hakipo kwenye orodha ya vyama vya siasa vilivyopo hapa nchini amesema hayo  wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, kushoto ni Mkurugenzi Utawala na Rasilimali watu Emmanule Kayuni,.
Wanahabari wakimsikilza kwa makini Msajili  Msaidizi wa ofisi ya msajili  wa Vyama  vya Siasa, Sisty Nyahoza leo Jiji Dar es Salaam.
 (Picha na Emmanue Massaka).
 
Na Chalila Kibuda,Globu ya Jamii
OFISI ya Msajili wa Vyama vya Siasa imesema kuwa Chama cha Tanzania People’s Party (TPP) kilifutwa, hivyo hakuna mtu mwenye mamlaka ya kutumia chama hicho katika uchaguzi mkuu wa mwaka huu.
 
Akizungumza na waandishi habari leo jijini Dar es Salaam, Msajili Msaidizi wa Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, Sisty Nyahoza amesema kuwa hivi karibuni kuna watu wameonekana katika chombo cha habari kimoja  sio Michuzi, wakiwajinasibu katika chama cha TPP wakati chama hicho kilishafutwa  toka 2001.
 
Nyahoza amesema kuwa watu wanaotumia chama hicho sheria itashika mkondo wake kwa kuwachukulia hatua watu kutumia chama ambacho kilishafutiwa usajili wa kudumu kwa msajili wa vyama vya siasa.
 
Aidha amesema kuwa vyama vilivyo katika usajili wa kudumu na vimeshiriki uchaguzi mkuu ni vyama 22 hivyo watu watambue chama cha TPP kilishafutwa kutokana na kukiuka kwa taratibu za ofisi ya msajili wa vyama vya siasa.
 
Nyahoza amesema kuwa watu wote wanaotumia vyama ambavyo usajili wake ulishafutwa  kwa mamlaka ya ofisi ya msajili wa vyama vya siasa watatachukuliwa hatua.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...