Ndugu Zangu Wana-DMV, Napenda kuchukua fursa hii kuwafahamisha kwamba tarehe 14/9/2015, niliteuliwa rasmi kuwa makamu mwenyekiti wa African Affairs Advisory Group (AAAG) iliyopo chini ya serikali ya kata ya Montgomery, Maryland (Montgomery County). 
Nafasi hii inausika na nyanja zote za maswala ya wahamiaji toka barani Afrika hususani; elimu,uchumi,uhamiaji, afya, tamaduni, bajeti,sera na miswada itakayoboresha huduma za jamii kwa Waafrika. 
Kutokana na majukumu haya, nimejiuzulu katika nafasi ya makamu wa rais wa jumuiya ya Watanzania Washington DC, Maryland na Virginia (DMV), nikiwa na imani kwamba nafasi hii itaniruhusu kuendeleza utumishi kwa jamii kwa kiwango kitakachowezesha na kuboresha ufumbuzi wa changamoto zetu hapa ugenini. 
Ndugu zangu, naomba mupokee shukrani zangu za dhati kwa ushirikiano wenu, upendo na kwa kunidhamini na nafasi nyeti ya makamu mwenyekiti DMV. 
Nafasi hii imenipa uelewa wa kina kuhusu changamoto za wana-Diaspora na mapungufu yaliyomo katika jamii zetu, ambayo yanahitaji mikakati itakayopelekea kupunguza vikwazo vya maendeleo yetu hapa ugenini. 
Mwisho niwashukurini tena na kuwakaribisha rasmi katika mikutano ya hadhara ya African Affairs Advisory Group, inayofanyika kila Alhamisi ya pili ya mwezi, kuanzia saa moja hadi saa mbili usiku (7:00pm- 8:00pm) 

Anwani;
1 Veterans Pl,
Silver Spring, 
MD. 20910- Civic Center. 
Asanteni sana, 
Harriet Shangarai 
Nipo Nanyi Daima!

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...