kushoto Mwenyekiti wa kamati ya tamasha la kuombea Amani hapa nchini,Alex Msama .

Na Mwandishi Wetu
MAASKOFU wa madhehebu mbalimbali na Wachungaji wanatarajiwa kushiriki kwenye Tamasha la Amani linalotarajiwa kufanyika Oktoba 4, mwaka huu Dar es Salaam.

Tamasha la Amani ambalo litahusisha waimbaji mbalimbali wa nyimbo za Injili ni maalum kwa ajili ya kuombea amani katika Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 25 mwaka huu.

Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa Dar es Salaam jana na Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya tamasha hilo, Alex Msama ilieleza kuwa maandalizi muhimu yanaenda vizuri.

“Niseme kwamba Maaskofu na Wachungaji mbalimbali wamekubali kujumuika nasi siku hiyo katika tukio muhimu, ambapo baada ya tamasha la Dar es Salaam tutaelekea pia mikoani,” alisema Msama.

Alisema wasanii mbalimbali wanaendelea kuomba kushiriki katika tamasha hilo alilosema litakuwa la aina yake.

 “Tunaandelea na mazungumzo na wasanii mbalimbali, ambapo tayari Rose Muhando ameshakubali kutumbuiza na wengine tuliowatangaza,” alisema Msama.

Baadhi ya wasanii maarufu ambao wamewahi kushiriki matamasha yanayoandaliwa na Msama ni Rose Muhando, Rebecca Malope, Christina Shusho, Upendo Nkone, Upendo Kilahiro, Solomon Mukubwa, Atosha Kissava, Ephraim Sekeleti na kundi la Glorious Celebration.

Pia kwaya mahiri ya Kinondoni Revival, Mwinjilisti Faraja Ntaboba kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Sohly Mahlangu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...