DAKTARI DHAMANA KANDA YA UNGUJA  DAKTARI FADHIL RAMADHAN AKITOA MAELEKEZO KWA MADAKTARI BINGWA KABLA YA KUANZA  ZOEZI LA MATIBABU KATIKA KIJIJI CHA KITOPE.
 DAKTARI FEI JIE AKIMPIMA MTOTO SARA SHAABAN MARADHI YA MENO NA KOO MKAZI WA KITOPE WILAYA YA KASKAZIN B”.
 PICHA NA ABDALLA OMAR - MAELEZO ZANZIBAR.

Mwashungi Tahir- Maelezo Zanzibar        14/09/2015
Jumla ya madaktari bingwa tisa kutoka nchini China Medical team wako Zanzibar kwa ajili ya kutoa huduma kila sehemu  mbalimbali hapa vijijini kwa ajili ya kuwarahisishia wananchi  kupata huduma ili waweze kuelewa kujua afya zao.

Hayo yamesemwa na daktari Dhamana  wa kanda ya Unguja DR Fadhil Mohammed Abdullah huko katika shehia ya Kaskazini B Kitope wakati wa zoezi hilo huko kijijini hapo.

Amesema lengo la madaktari hao kutoa huduma hiyo vijijini ni kuweza kuwarahisishia wananchi wa vijijini kuweza kupima na kujua afya zao ambapo zoezi hili hufanyika kila baada ya miezi mitatu na hutolewa bure.
Pia amesema madaktari hao wapo nchini wakishirikiana na madaktari wa wizara ya Afya  kwa kutoa huduma hizo huko kijijini  na wanachi kuweza kujitambua afya zao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...