Mgombea wa urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia CCM Dkt. John Pombe Magufuli akihutubia umati wa watu kwenye mkutano wa kampeni uliofanyika katika uwanja wa Jamhuri mjini Dodoma leo, akiendelea na kampeni zake za kuisaka Ikulu nchini Kote huku akiwaomba Watanzania kumpigia kura za ndiyo ifikapo Oktoba 25 mwaka huu katika uchaguzi wa Rais, Wabunge na Madiwani ili aweze kuwatumikia kwa uaminifu mkubwa.

Akitoa hotuba yake katika moja ya mikutano  yake alioufanya katika mji wa Kibaigwa Dk. John Pombe Magufuli amesema hakuna kitu kinachomuumiza kama mauaji ya wakulima na wafugaji yanayotokea kati ya wilaya za Kongwa Mkoani Dodoma na Kiteto  mkoani Manyara.

Dkt Magufuli ameahidi kuwa mara baada ya kuchaguliwa  na kuunda Serikali yake,jambo hilo atalipa uzito wa juu na kulifanyia kazi kwa umakini mkubwa. “Yaani Mimi Magufuli Nimteuwe Waziri na watendaji wengine wa serikali halafu Mauaji yatokee watu wafe, Mkuu wa mkoa yupo , Mkuu wa wilaya yupo  na Kamanda wa Polisi yupo wabaki wanapunga upepo, wamiliki wa Ng’ombe wabaki  wanakula maisha haiwezekani,nitalala nao mbele na  Ng’ombe wataliwa msibani kwa uzembe waliousababisha”,alisema Magufuli kwa msisitizo mkubwa.

Magufuli amewataka wafugaji na wakulima kuishi kwa amani bila kubaguana, lakini pia akasema atatumia sheria za ardhi na kuhakikisha maeneo ya wafugaji na wakulima yanatengwa, ili wafanye shughuli  zao na kukuza kipato na  uchumi wao bila kusumbuliwa. 
 Baadhi ya wananchi wa mji wa Dodoma na vitongoji vyake wakimsiiliza Dkt Magufuli alipokuwa akinadi sera zake za kuomba kura ili kushika nafasi  ya Urais ya awamu ya tano.

  Waziri Mkuu wa zamani, Jaji mstaafu Joseph Warioba, akimnadi Dkt.Magufuli ambapo alimfagilia kwa kuhubiri amani katika mikutano yake ya kampeni kuliko,na pia amewaasa vijana kuilinda amani ya nchi iliopo kwa gharama yoyote,kuishi bila kubaguana. 
 Dkt. Magufuli akimnadi mgombea Ubunge wa Dodoma Mjini,mara baada ya kumkabidhi Ilani ya Uchaguzi ya CCM, Ndugu Anthony Mavunde wakati wa mkutano wa kampeni kwenye Uwanja wa Jamhuri mjni Dodoma leo.
  Dk Magufuli akimnadi Mgombea ubunge Jimbo la Mpwapwa, George Lubeleje,mjini MPwapwa katika uwanja wa mgambo.
 Mgombea urais wa Tanzania kupitia CCM, Dk John Magufuli akimnadi Mgombea ubunge Jimbo la Kongwa, Naibu Spika wa Bunge, Job Ndugai wakati wa mkutano wa kampeni jimboni humo.
  Mawaziri wakuu wa zamani, John Samuel Malecela na Jaji Mstaafu Joseph  Sinde Warioba wakifuatilia mkutano wa kampeni wa Dkt Magufuli alipokuwa akiwahutubia wananchi wa Dodoma kwenye mkutano wa kampeni. 
  Dk Magufuli akijipigia kampeni  kwa wakazi wa Kibaigwa , wilayani Kongwa leo.Akiwa wilayani Kongwa, Dk Magufuli amesema kuwa akishinda urais atahakikisha anadhibiti mapigano  kati ya wakulima na wafugaji yanayoendelea nchini na kusababisha vifo vya watu wengi 
  Dkt. Magufuli akiwapungia mikono wananchi alipowasili kwenye kampeni Uwanja wa Jamhuri Dodoma leo.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Magufuli semaa
    Semaa usiogope semaaa
    Magufuli sema
    Sema usiogope semaa
    Sisi vijana.......

    ReplyDelete
  2. Wiki ya mwisho ya Oktoba watasoma namba CCM mbele kwa mbele

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...