Makamu wa Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiangalia
moja ya jiwe lenye Madini huku akipata maelezo kutoka kwa Mkurugenzi wa
Kampuni ya Aifola Investiment Co. Ltd, Zubery Mabie, kuhusu upatikanaji
wa madini na utengenezaji wa Unga wa 'Lime Powder', wakati Makamu
alipokuwa akitembelea Mabanda ya maonesho kwenye ufunguzi wa Kongamano
la Uwekezaji wa Ziwa Tanganyika, lililofanyika leo Sept 9, 2015 kwenye
Hoteli ya Tanganyika Mjini Kigoma.
Sehemu
ya washiriki wa Kongamano hilo wakimsikiliza Makamu wa Rais Dkt. Bilal,
alipokuwa akihutubia kwenye ufunguzi wa Kongamano hilo.
Makamu
wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal,
akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya viongozi na baadhi ya
washiriki wa Kongamano hilo waliohudhuria Kongamano hilo baada ya
ufunguzi, uliofanyika leo Sept 9, 2015. Picha na OMR
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...