Afisa Mawasiliano wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF), Fausta Msokwa akiongea na waandishi wa habari mapema leo asubuhi jijini Dar es Salaam juu ya maadhimisho ya miaka nane ya mafanikio ya TMF. Pembeni ni Mkurugenzi wa TMF, Ernest Sungura na Afisa Mafunzo wa TMF, Radhia Mwawanga.
Mkurugenzi wa Mfuko wa Vyombo vya Habari Tanzania (TMF), Ernest Sungura akiongea kwenye mkutano na waandishi wa habari kutangaza tukio hilo, alisema Tarehe 22 Septemba, 2015 tutakuwa na tukio la madhimisho ambayo yatajumuisha maonyesho kwa ajili ya waandishi wa habari waliowezeshwa na misaada ya TMF kuonyesha kazi zao na jinsi gani zimechangia kuleta uwajibikaji na pia kuonyesha kazi ambazo zimepandisha kiwango cha mijadala ya umma katika masuala husika hususani utawala bora na haki za binadamu pamoja na sherehe ya utoaji tuzo kwa waandishi waliowezeshwa na TMF na kazi zao kuweza kuleta mabadiliko chanya.
Hizi simu kweli! Hata kwenye meza kuu, wenzio wanaelezea mambo wewe upo busy FB! Tut afrika tu!
ReplyDelete