Mgombea Ubunge kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM) jimbo la Kibamba Dkt Fenella Mukangara akiongea na wakazi wa eneo hilo wakati akipokuwa akitangaza sera za chama chake na kuwaomba wampigie kura katika uchaguzi ujao pamoja na madiwani wengine sita wa chama cha mapinduzi.Dkt Fenella alitaja vipaumbele vyake katika jimbo hilo ambavyo ni Maji,Elimu,Afya pamoja na ajira kwa Vijana na kuwasihi wakazi hao kuchagua maendeleo bora yatayopatikana ndani ya CCM.
Mwenyekiti  wa CCM mkoa wa Dar es Salaam Bw.Salum Madenge akimnadi  Mgombea Ubunge jimbo jipya la kibamba  Dkt Fenella Mukangara(waliokaa aliyesuka) kwa wakazi wa kibamba leo hii jijini Dar es Salaam.Bw Madenge aliwasisitiza wakazi wa jimbo ilo kumchagua Bi Fenella kwani ni mtu shupavu,mwenye kupenda maendeleo na mzalendo
 Mmoja wa wakazi wa kibamba aliyejitokeza kumsikiliza Mgombea Ubunge kwa Tiketi ya CCM akiwa amenyanyua bango lenye ujumbe maalum kumhusu mgombea jijini Dar es Salaam.
 
 Wakazi wa kibamba waliojitokeza kwa wingi wakimskiliza kwa makini mgombea ubunge jimbo la kibamba Dkt Fenella Mukangara akinadi sera zake pamoja na Mgombea uyo kutaja vipaumbele kwa jimbo ilo kuwa ni Maji,Elimu,Afya na ajira kwa Vijana.
Wakazi wa kibamba waliojitokeza kwa wingi wakimskiliza kwa makini mgombea ubunge jimbo la kibamba Dkt Fenella Mukangara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...