Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam
Hatua thabiti za utekelezaji wa maazimio ya mkutano wa Nane wa Baraza la Biashara la Taifa (TNBC) zinatarajiwa kujulikana wiki chache zijazo.

Maazimio hayo yanalenga hasa kuimarisha mazingira ya biashara nchini na sekta ya utalii.

Akiongea na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa TNBC, Bw. Raymond Mbilinyi (Pichani) alisema hatua za utekelezaji maazimio mbalimbali ya kuimarisha sekta hizo zitajulikana katika mkutano wa 9 wa baraza hilo unaotarajiwa kufanyika tarehe 2 mwezi ujao (Oktoba).

“Mapendekezo mengine ni ya kiutawala zaidi ambayo ni rahisi lakini kuna maswala mengine yatahitaji mabadiliko ya sheria mbalimbali na haya yatatakiwa kufuata taratibu zinazotakiwa,” alisema Bw. Mbilinyi na kumshukuru Rais Kikwete kwa kuendesha mkutano huo.

Akielezea baadhi ya maeneo yanayohitaji kuboreshwa alisema kuwa pamoja na kuwa na kitengo maalum cha kuhakikisha watanzania wanashiriki kikamilifu katika ujenzi wa uchumi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...