Na Mwandishi wetu, Dar es Salaam
Hatua
thabiti za utekelezaji wa maazimio ya mkutano wa Nane wa Baraza la
Biashara la Taifa (TNBC) zinatarajiwa kujulikana wiki chache zijazo.
Maazimio hayo yanalenga hasa kuimarisha mazingira ya biashara nchini na sekta ya utalii.
Akiongea
na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, Katibu Mtendaji wa
TNBC, Bw. Raymond Mbilinyi (Pichani) alisema hatua za utekelezaji maazimio
mbalimbali ya kuimarisha sekta hizo zitajulikana katika mkutano wa 9 wa
baraza hilo unaotarajiwa kufanyika tarehe 2 mwezi ujao (Oktoba).
“Mapendekezo
mengine ni ya kiutawala zaidi ambayo ni rahisi lakini kuna maswala
mengine yatahitaji mabadiliko ya sheria mbalimbali na haya yatatakiwa
kufuata taratibu zinazotakiwa,” alisema Bw. Mbilinyi na kumshukuru Rais
Kikwete kwa kuendesha mkutano huo.
Akielezea
baadhi ya maeneo yanayohitaji kuboreshwa alisema kuwa pamoja na kuwa na
kitengo maalum cha kuhakikisha watanzania wanashiriki kikamilifu katika
ujenzi wa uchumi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...