RAIS wa awamu ya kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati baba
wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere alizaliwa mwaka 1922 katika Wilaya ya Butiama Mkoa wa Mara, mnamo tarehe 14 Oktoba, 1999, aliaga
dunia katika hospitali ya mtakatifu Thomas
Jijini London
nchini Uingereza.
Katika uhai wake, alikuwa ni Mmalenga.
Aliandika barua ya Kiserikali kwa mtindo
wa utenzi, pia alijibiwa barua hiyo kwa mtindo
wa utenzi na Nguli/Karii, Hayati Saadani
Abdul Kandoro aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo mnamo mwaka 1964.
Nukuu ya Hayati Saadani A. Kandoro “Huu ni utenzi ulioandikwa kwa njia ya barua iliyotungwa na Muheshimiwa
Mtukufu mwalimu J.K. Nyerere President
wa TANU na Serikali. Aliniletea barua hiyo ili kunizungumza jinsi ya watu
wanaopenda kujisaidia katika shughuli za maendeleo na jinsi ya kuwapa moyo
dhidi ya adui wa jamii katika shughuli za vijiji”.
Picha ya Hayati Mw. J.K. Nyerere
SHEIKH KANDORO, SIKIA!
1.
Sheria husaidia,
Kuijenga
Tanzania,
Siyo kazi
ya sheria,
Nchi kutuharibia.
2.
Kila
nchi ina nia,
Inayoikusudia,
Vile vile
ina njia,
Itakayoipitia.
3.
Tanzania
tuna nia,
Ya kujenga
ujamia,
Na njia ya kupitia,
Ni wote kusaidia.
4.
Kijiji
cha turadhia,
Kisima
kujipatia,
La magambo
limelia,
Watu wakahudhuria.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...