RAIS wa awamu ya kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere  alizaliwa mwaka 1922 katika  Wilaya ya Butiama Mkoa wa  Mara, mnamo tarehe 14 Oktoba, 1999, aliaga dunia katika hospitali ya mtakatifu  Thomas  Jijini London  nchini Uingereza.  

Katika uhai wake,  alikuwa ni Mmalenga.   
Aliandika barua ya Kiserikali kwa mtindo wa utenzi, pia alijibiwa barua hiyo  kwa mtindo wa utenzi na Nguli/Karii,  Hayati Saadani Abdul Kandoro aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo mnamo mwaka 1964.

Nukuu ya Hayati Saadani A. Kandoro “Huu ni utenzi ulioandikwa kwa njia ya barua iliyotungwa na Muheshimiwa Mtukufu mwalimu J.K. Nyerere  President wa TANU na Serikali. Aliniletea barua hiyo ili kunizungumza jinsi ya watu wanaopenda kujisaidia katika shughuli za maendeleo na jinsi ya kuwapa moyo dhidi ya adui wa jamii katika shughuli za vijiji”.
 Picha ya Hayati Mw. J.K. Nyerere

                       SHEIKH KANDORO, SIKIA!
1.     Sheria  husaidia,
Kuijenga Tanzania,
Siyo kazi ya sheria,
     Nchi kutuharibia.

2.     Kila nchi ina nia,
Inayoikusudia,
Vile vile ina njia,
   Itakayoipitia.

3.     Tanzania tuna nia,
Ya kujenga ujamia,
Na  njia ya kupitia,
  Ni wote kusaidia.

4.     Kijiji cha turadhia,
Kisima kujipatia,
La magambo limelia,
  Watu wakahudhuria.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...