PATASHIKA ya michuano ya vijana chini ya miaka 12 ya Airtel Rising Stars ngazi ya
taifa, imeendelea kutimua vumbi katika dimba la Kumbukumbu ya Karume
jijini Dar es Salaam, ambapo timu za Temeke na Mwanza zilipepetana kwa
upande wa wasichana huku Mwanza na Morogoro walitifuana vikali kwa
upande wa wavulana.
Kwa
kuanzia na mchezo ambao ulizikutanisha timu za wavulana, Mwanza
waliwasambaratisha vibaya Morogoro kwa kuwashindilia magoli 3-1.
Mwanza ambao walionekana kutakata kila idara, walijipatia bao la uongozi
mnamo dakika ya 30 kupitia Lazaro Richard, baada ya kuitokea pasi nzuri
iliyopigwa na David Richard na kumchambua vizuri kipa wa Morogoro kisha
kuukwamisha mpira huo kimiani.
Morogoro
ambao katika mchezo wa Jumatatu wiki hii, waliitandika Kinondoni mabao
2-1, waliamka kutoka usingizi na kufanya mashambulizi kadhaa ambayo
hata hivyo hayakuzaa matunda.
Alikuwa ni David Richard ambaye aliandikia Mwanza bao la pili mnamo dakika ya 54, kutokana na krosi safi iliyochongwa kutoka mashariki mwa uwanja na kuusindikiza kwa uzuri kabisa mpira huo langoni mwa Morogoro.
Alikuwa ni David Richard ambaye aliandikia Mwanza bao la pili mnamo dakika ya 54, kutokana na krosi safi iliyochongwa kutoka mashariki mwa uwanja na kuusindikiza kwa uzuri kabisa mpira huo langoni mwa Morogoro.
Baada
ya goli hilo, Morogoro waliamka na kupeleka mashambuliza ya mara kwa
mara langoni mwa Mwanza, na ndipo mshambuliaji wao hatari Evidence
Kiongozi alipofunga goli dakika ya 63 na kuamsha matumaini ya walau
kusawazisha na hatimaye kutafuta goli la ushindi.
Mambo yalizidi kuwa mabaya kwa upande wa Morogoro, baada ya David
Richard kwa mara nyingine tena, kuifungia Mwanza bao la tatu na mwisho
katika mchezo huo mnamo dakika ya 68 na kuhitimisha karamu ya magoli kwa
upande wa timu yake.
Katika mchezo mwingine, wasichana wa Temeke waliwaadabisha vikali Mwanza
kwa kuwafumua magoli 3-0.
Temeke
ambao katika mchezo wao wa kwanza walitaoa kipigo cha mbwa mwizi cha
magoli 8-0 dhdi ya Arusha, walianza kupata bao mnamo dakika ya 11 baada
ya Shamimu Khamisi kufunga goli maridhawa, baada ya kutokea rapsha
langoni mwa Mwanza na kuipa timu yake goli la uongozi.
Iliwachukua takribani dakika takraibani 28, Temeke wakapata bao la pili kupitia kwa Rose Mpoma baada ya kuachia shuti kali la mbali na kuzama moja kwa moja wavuni, na kumwacha mlinda mlango wa Mwanza asijue la kufanya langoni mwake. Mpaka timu hizo zinakwenda mapumzikoni, Temeke walikuwa mbele kwa magoli 2-0.
Iliwachukua takribani dakika takraibani 28, Temeke wakapata bao la pili kupitia kwa Rose Mpoma baada ya kuachia shuti kali la mbali na kuzama moja kwa moja wavuni, na kumwacha mlinda mlango wa Mwanza asijue la kufanya langoni mwake. Mpaka timu hizo zinakwenda mapumzikoni, Temeke walikuwa mbele kwa magoli 2-0.
Temeke
waliendeleza kilio kwa wapinzani wao, katika kipindi cha pili kwa
kushindilia msumari wa tatu na wa mwisho mnamo dakika ya 56, baada ya
Oppah Masoud kugongeana mpira vizuri na Rose Mpoma na hatimaye
kuusukumiza moja kwa moja mpira kimiani.
Baada
ya kupata goli la tatu, Temeke walionekana kuridhika na kucheza kwa
kijiamini huku wakisubiri kipenga cha mwisho cha mwamuzi, huku wakiwa
wamejikunyajia pointi tatu kibindoni.
Patashika ya michuano ya vijana chini ya miaka 12 ya Airtel Rising Stars ngazi ya taifa,
Patashika ya michuano ya vijana chini ya miaka 12 ya Airtel Rising Stars ngazi ya taifa baina ya Mwanza na Morogoro
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...