Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Mhandisi Mussa Natty wapili (kushoto) akiwakabidhi ufagio Mwenyekiti wa bodi wa Benki ya Covenant Balozi, Salome Sijaona, wa pili (kulia) na Mkurugenzi Mtendaji wa benki hiyo, Sabetha Mwambenja wakati Uzinduzi wa kampeni ya kupambana na kipindupindu katika Manispaa hiyo ambapo benki hiyo imetoa basi kuwatembeza wananchi waliojitolea kutoa elimu kuhusu ugonjwa wa Kipindupindu na kufanya usafi, kulia ni Mratibu wa Federation Taifa, Khadija Kingi.
Mkurugenzi Mtendaji wa benki ya Covenant, Sabetha Mwambenja, wapili (kushoto) akimkabidhi gari Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni, Mhandisi Mussa Natty wapili (kulia) kwaajili ya Wanachama wa Taasisi ya Federation waliojitolea kutoa elimu elimu ya  ugonjwa wa Kipindupindu na kufanya usafi katika Manispaa hiyo (kulia) Mwenyekiti wa bodi wa Benki hiyo Balozi, Salome Sijaona na Mratibu wa Federation Taifa, Khadija Kingi.
Mwenyekiti wa bodi wa Benki ya Covenant Balozi, Salome Sijaona, kwa Pamoja na Mkurugenzi wa Benki hiyo Sabetha Mwambenja(Kushoto) wakikabidhi vinywaji kwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Kinondoni Mhandisi Mussa Natty, na Mratibu wa Taasisi ya Federation Taifa Khadija Kingi, Ikiwa ni sehemu ya kuwezesha kampeni ya kupambana na kipindupindu kwa Manispaa hiyo.

 Manispaa yazindua mpango wa kukitokomeza
BENKI ya Covenant imetoa msaada wa basi maalumu kwa ajili ya kuwasafirisha wanachama wa taasisi ya Federation waliojitolea kufanya usafi na kutoa elimu kwa ajli ya kutokomeza ugonjwa wa kipindupindu katika manispaa ya Kinondoni iliyoko jijini Dar es salaam.

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Covenant bank, Balozi Salome Sijaona amesema kuwa benki hiyo imekuwa Msitali wa mbele katika kuisaidia jamii ya Watanzania wasio katika sekta Rasmi ambao kwa kiasi kikubwa ndio wanaoishi katika Mazingira magumu na hatarishi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hiki kipindipindu tunatakiwa kukiondoa kiwe tu kwenye vitabu vya historia kwamba enzi hizo kilikuwepo. Tujiwekee mikakati hatuhitaji kuwa nacho, kama ni elimu ya usafi tupewe kila mahali.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...