Image result for HIFADHI  YA  JAMII


           
Na Bashir Yakub

Hela  ya  mifuko  ya  hifadhi ya jamii  ni  hela  ambayo  mwajiriwa  hukatwa  kiasi  kadhaa katika  mshahara  wake na  mwajiri  hutoa  kiasi  kadhaa  na  kuhifadhiwa  katika  mfuko uitwao  mfuko  wa hifadhi ya  jamii. Mfuko  wa  hifadhi  ya jamiii ni  kama NSSF, PSPF, LAPF, GEPF  n.k. Hii ndio  mifuko  ya  hifadhi  ya   jamii. Ipo  mifuko  ya  hifadhi  ya jamii  ambayo  huhudumia  mashirika  ya  umma  na  ipo  mingine  ambayo  huhudumia  mashirika  binafsi, makampuni  binafsi  na  sasa  ipo  inayohudumia  hata wajasiriamali  wadogo  ambao  sio  kampuni  wala  shirika.
Lengo  kuu  ni  kumpunguzia  mtumishi  au  mfanyakazi  machungu  ya  maisha pindi  anapostaafu  au  kuacha   kazi.  Ni  kumwezesha  mtu   kuweza  kukabiliana  na  maisha  yake  baada  ya  kutokuwa  na  kazi  iliyokuwa  ikimwingizia  kipato. Ni  kumfanya  asikose  hata  matumizi  ya  kawaida  kama  chakula, malazi, mavazi   na  hata  matumizi  kama  ada  za  shule  ,matibabu  n.k. Mifuko    hii  haipo  Tanzania tu  bali  ni  ajenda  ya  dunia.  Ukienda  ulaya, Amerika, Asia  na  kote  Afrika utaikuta.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Naomba muwasiliane na SSRA kwani hizo taarifa CHANZO CHAKE SIO SSRA.
    Mifuko yote ya hifadhi ya jamii Tanzania hu hudumia Watanzania wote bila kujali ni mwajiriwa wa sekta ramsi au sekta isiyorasmi.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...