THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA

DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS
Telephone: 255-22-2114512, 2116898
Website : www.ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425



PRESIDENT’S OFFICE,
      STATE HOUSE,
              1 BARACK OBAMA ROAD,  
11400 DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
 

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Serikali ya Awamu ya nne inayomaliza muda wake mwezi Octoba mwaka huu, imeyashughulikia matatizo yaliyokuwepo kwa kiasi kikubwa na yale ambayo bado kukamilika, utekelezaji wake unaendelea na mengine mipango imekwisha anza.

Rais Jakaya Mrisho Kikwete amesema hayo jana mjini Kigoma katika uwanja wa Tanganyika, kwenye mkutano wa hadhara kwa madhumuni ya kuagana na wananchi wa Kigoma.

"Mlinichagua, mlinipa imani yenu, sikusahau kwa sababu nilikua naifahamu Kigoma, kilio chenu nilikuwa nakifahamu".  Rais amewaambia wananchi waliofurika uwanjani hapo.

Matatizo yaliyokuwepo Mkoani Kigoma wakati Rais Kikwete anaingia madarakani mwaka 2005 ni pamoja na tatizo la umeme ambapo serikali ilinunua jenereta na kulifunga Mkoani Kigoma.

Jenereta hilo lilitatua matatizo ya umeme katika miji ya Kasulu, Kibondo na Kigoma Ujiji.

Awamu ya pili ya utatuaji wa matatizo ya Umeme, yanatatuliwa chini ya Mradi wa Umeme Vijijini, maarufu kama Rural Electrification Agency (REA), ambao umekua na lengo la kuunganisha vijiji vilivyobakia.

Tayari vijiji 92 vimeunganishwa  na hatimaye vijiji 306 vya Mkoa mzima vitaunganishwa. Awamu hii itahusisha Ujenzi wa kituo cha kuongeza nguvu ya umeme na hatimaye umeme kufika Wilaya zingine za Uvinza, Buhigwe na Kakonko.

Tatizo lingine lilokuwepo ni Maji ambapo Rais Kikwete amesema Mradi mkubwa unaofadhiliwa na Jumuiya ya Ulaya unatarajia kukamilika mapema mwakani

Mkoa wa Kigoma pia umekua na tatizo la Mawasiliano ambapo, mwaka 2005 wakati Rais Kikwete anaingia madarakani, Mkoa ulikua na barabara moja ya lami yenye urefu wa kilomita 7.36, Hivi sasa kuna barabara za lami zenye kilomita 28.7 Kigoma mjini, Kasulu kilomita 1.5 na Kibondo kilomita 2.7.

Mbali na barabara za mjini, serikali ya awamu ya nne imeunganisha Mkoa wa Kigoma na Mikoa jirani kwa kujenga barabara kwa kiwango cha lami. Barabara hizo ni za Kigoma-Kidahwe km 28.2, Mwadiga-Manyovu km 60 na Kidahwe Uvinza km 76.6 na ujenzi ukiwa bado unaendelea kwa barabara za Kidahwe-Kasulu km 50, Nyakanazi- Kakonko-Kabingo km 75.

Leo tarehe 15 Septemba, Rais Kikwete anatarajia kuzindua daraja la Kikwete katika Mto Malagarasi lenye urefu mita 275 na barabara zake unganishi zenye urefu wa km 48. Rais pia atazindua barabara ya Kidahwe-Uvinza yenye urefu wa km 76.6 ambayo  imejengwa kwa kiwango cha lami.

Imetolewa na :
Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais, Msaidizi,
Ikulu-Kigoma
15 Septemba, 2015

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...