Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha CCM,Dkt Magufuli akiwasalimia maelfu ya Wananchi waliofika katika uwanja wa Barafu mjini Igunga,Dkt Magufuli aliwahutubia wananchi hao.
 Mgombea Urais kwa tiketi ya CCM Dk.John Magufuli akisisitiza mbele ya maelfu ya Wakazi wa mji wa Igunga jioni ya leo kwenye mkutano wa hadhara kuwa Serikali ya awamu ya tano itajenga viwanda mbalimbali vikiwamo viwanda vya nguo ikiwa ni mkakati wa kuinua zao la pamba ambalo linalimwa kwa wingi mikoa ya kanda ziwa,amesema kuwa Serikali yake imedhamiria kuleta mabadiliko bora na si bora mabadiliko na kuongeza kazi kubwa atakayofanya ni kusimamia vema rasilimali za nchi kwa maslahi ya Watanzania wote.
 Dkt Magufuli kwa nyakati tofauti kwenye mikutano ya hadhara akiwa katika wilaya ya Maswa na kisha jimbo la Kishapu na Igunga, Dk.Magufuli amesema kuwa anatambua umuhimu wa kuwa na viwanda nchini na hivyo serikali yake itasimamia ujenzi wa viwanda kwa lengo la kuimarisha uchumi na wakati huo huo kusaidia wakulima na wafugaji kunufaika na shughuli wanaofanya nchini.   
  Dk Magufuli akizungumza na wananchi wakati akijinadi  mjini Malampaka, Maswa, ambapo alisema akishinda urais ataanzisha viwanda vingi ili kuongeza thamani ya mazao nchini.
 Dk Magufuli akihutubia wananchi katika Mji wa Maganzo mkoani Shinyanga, ambapo aliomba kumpigia kura ali ashinde awasaidie kuboresha sekta ya uchimbaji madini kwa serikali kuwakopesha wachimbaji wadogo wadogo  kwa kuwapatia mitaji  na vifaa. 


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. It is the time for Tanzanians to elect their leaders no one from outside should try and meddle in anyway on the electioneering process because this amounts to usurping the role of the electrolate.

    Nyerere did speak out against foreigners who wanted to meddle in Tanzanian politics and asked why, how will they be paid? this question still remains for those who will not keep off. Foreigners can observe the process when time comes, but not seek to facilitate any candidate by engaging them or financially supporting them. If a foreigner for example is planning to do this by funding motor riders he is trying to influence an election contrary to the wishes of the citizenry and the public good of Tanzanians. It is curious when in his own country he has motor cycles that he is not supporting in the same way. General caution: Interfering in the election process of another country is interfering in the internal affairs of the country it is wrong.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...