Na Magreth Kinabo- maelezo
SERIKALI imesema kwamba imeshalipa madeni ya walimu ya kiasi cha Sh. bilioni 5.7 ambayo yaligungulika kihalali kati ya Sh. bilioni 19.6 zilizokuwa zinadaiwa kudaiwa,hivyo kwa sasa hakuna malalamiko mwalimu ambaye hajalipwa.
Aidha Serikali imependekeza kwamba halimashauri zilizowasilisha madeni ambayo si halali, yenye shaka, au watumishi wasio na madai, madai ya watumishi wasio na madai, madai ya watumishi waliokwishalipwa na waliowasilisha madai ya mishahara kama madai yasiyo ya mishahara wawajibishwe.
Kauli hiyo imetolewa leo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha, Dkt. Servacius Likwelile wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kwenye ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo jijini Dar es Salaam.
Dkt. Likwelile alisema hayo wakati akitoa taarifa ya uhakiki wa madeni ya walimu wa shule za msingi, sekondari na Watumishi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...