Na Magreth Kinabo- maelezo
SERIKALI imesema kwamba imeshalipa madeni ya walimu  ya kiasi cha Sh. bilioni 5.7 ambayo yaligungulika kihalali kati ya Sh. bilioni 19.6 zilizokuwa zinadaiwa kudaiwa,hivyo  kwa  sasa hakuna  malalamiko mwalimu ambaye hajalipwa.

Aidha Serikali imependekeza kwamba   halimashauri  zilizowasilisha  madeni ambayo si  halali, yenye shaka, au watumishi wasio na madai, madai ya watumishi wasio na madai, madai ya watumishi waliokwishalipwa na waliowasilisha madai ya mishahara kama madai yasiyo ya mishahara wawajibishwe.

Kauli hiyo imetolewa leo na Katibu Mkuu wa Wizara ya  Fedha, Dkt. Servacius Likwelile wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu kwenye ukumbi wa mikutano wa wizara hiyo jijini Dar es Salaam.

Dkt.  Likwelile  alisema hayo wakati akitoa taarifa  ya  uhakiki wa madeni ya  walimu wa shule za msingi, sekondari na  Watumishi wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya  Ufundi Stadi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...